Mwenyekiti wa Peacock Hotel,Joseph Mfugale (kulia) akizungumza leo katika uzinduzi wa usiku Mtanzania uliofanyika katika hotel ya Peacock,jijini Dar asubuhi hii.kushoto ni Mkurugenzi Muendeshaji wa Hotel hiyo,Damas Mfugale.
Meneja Masoko wa Precision Air,Emillian Rwejuna akisisitiza jambo katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika Hotel ya Peacock,jijini Dar.
Baadhi ya wawakilishi wa makampuni yaliyojitokeza kufanikisha usiku huo wa Mtanzania,toka kulia ni Meneja Masoko wa Tanzania Distilleries Ltd,Martha Bangu,Meneja wa Benki ya Posta,Noves Mosses,Meneja Masoko wa Precision Air,Emillian Rwejuna pamoja na Mwenyekiti wa Peacock Hotel,Joseph Mfugale.Shoo hii inaratibiwa na kampuni ya 1Plus Communications Ltd.
Baadhi ya wanahabari waliohudhuria katika mkutano huo wa uzinduzi wa Usiku wa Mtanzania.

======= ======= =======

Peacock Hotel ni hoteli inayojali wateja wake kwa kiwango cha juu. Ili kudumisha na kuendeleza mila, desturi, na utamaduni wa mtanzania, hoteli ilianzisha Usiku wa Mtanzania ambapo vyakula vya asili ya Tanzania vinaandaliwa kwa ladha ya asilia. Ni hoteli pekee nchini Tanzania ambayo inadumisha menu halisi ya kitanzania.

Usiku huu unatimiza miaka kumi(10) mwaka huu tangu uanzishwe. Kila Jumatano usiku panakuwepo vyakula vya kitanzania vya aina mbalimbali na makabila mbalimbali. Mandhari ya hotel hugeuka kuwa ya asili ili kuleta maana halisi ya lengo la usiku huu.

Tarehe 3.12.2010 ni siku ya kusherehekea kutimiza miaka kumi ya Usiku wa Mtanzania katika ukumbi wa Karimjee kuanzia saa 12:00 jioni hadi saa 6:00 usiku.

Shamrashamra hizo zitapambwa na ngoma za asili pamoja na muziki kutoka kwa Kidum-Kenya, Lady Jay Dee, Sikinde-Ngoma ya Ukae, na Waane Star.

Tunapenda kutoa shukrani za dhati kwa wateja wetu wote ambao wanaendelea kuburudika kwa milo ya kitanzania pamoja na burudani za asili. Kwa kutambua uwepo wao na kuthamini usiku huu tunawaahidi huduma bora zaidi na siku ya sherehe tutawatambua rasmi baadhi yao kwa niaba yaw engine kwa kuwapa zawadi.

Washiriki wenzetu katika kuunga mkono Usiku wa Mtanzania kutimiza miaka kumi ni Benki ya Posta, Shear Illussion, Vayle Springs, na Precision Air. Hawa wanadhihirisha dhamira yao ya kuunga mkono mila na desturi za kitanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hongereni PEACOCK kwa kutimiza miaka kumi na kutoa huduma bora zaidi.La pili ni kwa kukumbuka utamaduni wetu maana kwa sasa tanzania tumeathiriwa na umagharibi zaidi.nimefurahi kusikia sikinde ngoma ya ukae watakuwepo pia, hivi wadau mnaofahamu ni wapi wazee hawa wa sikinde wanaburudisha mwishoni mwa wiki mnijulishe tafadhali.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...