tovuti ya school of law-udsm kwishnei...?

habari za kazi na shukrani kwa kutuhabarisha kwa kutumia blog.

naleta malalamiko yangu kuhusu tovuti ya school of law (zamani faculty of law) ya chuo kikuu cha dar es salaam. tovuti hii ina zaidi ya miezi sita sasa ipo under construction. watu tunataka habari za chuo aidha kujiunga kwa kozi mbali mbali au kujua habari mbali mbali lakini tunatatizwa na kukosekana kwa tovuti hiyo.

inashangaza na kusikitisha kuwa zaidi ya miezi sita tovuti hiyo ipo matengenezoni... jee wahusika wanalijua hili? jee wanajenga tovuti au ghorofa la makaazi na ofisi?

ustaarabu ungewafanya kuimaintain tovuti ya awali ya faculty of law kabla ya kuifuta wakati wanaendelea kuitengeneza hiyo ya school of law ili kutokatisha wananchi na wadau habari kwa muda mrefu. tunaomba wahusika walitafutie ufumbuzi tatizo hili.

mdau wa elimu ya juu
tanzania
-----------------------------
University of Dar-es-Salaam
School of Law (Formally Faculty of Law)
P.O.Box 35093
Dar-es-Salaam, TANZANIA.
Telephone:+255-22-2410 254
Fax:+255-22-2410 672
Telegram:UNIVERSITY DAR-ES-SALAAM
E-mail: dean_law@udsm.ac.tz, laws@ucc.ac.tz
Website: http://law.udsm.ac.tz/

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 12 mpaka sasa

  1. mdau ingia humu http://www.lst.ac.tz/

    ReplyDelete
  2. most of these so called tovutis are not functioning you should visit personally to find out what you want.

    ReplyDelete
  3. Mdau pamoja na malalamiko yako naomba nikufahamishe kwamba School of Law na Faculty of Law ni vitu viwili tofauti kabisa na majukumu yao ni tofauti. School of law imeanza karibuni na inachukua graduate lawyers kwa ajili ya kuwapa "practical side ya law" ili kuwatayarisha kufanya kazi. Majukumu ya faculty bila shaka unayajua na unafahamu kwamba ipo miaka mingi sana.

    ReplyDelete
  4. mdau wa kwanza mtoa hoja anakusudia school of law ya chuo kikuu dsm sio school of law ya tanzania. hii ya chuo kikuu dsm awali ilikuwa faculty of law. ukiingia katika web ya chuo kikuu ukienda katika link inayokuunganisha ni hiyo web utakutana na maandishi under construction.

    hii ya chuo kikuu hutoa kozi za kawaida kama bachelor masters na phd degrees kama ilivyokuwa faculty. hii web uliyotoa wewe ni law school inayotoa mafunzo ya vitendo kwa wahitimu wa sheria wanaotaka kuwa mawakili. haitoi master, bachelors wala phd.

    ReplyDelete
  5. mdau wa kwanza umechemsha. hiyo sio aliyokusudia mtoa hoja. aliyokusudia yeye ni www.law.udsm.ac.tz hebu ingia uone huo uozo wa chuo kikuu cha dsm.

    rekebisheni makosa enyi chuo kikuu

    ReplyDelete
  6. Hao watu hawapo makini na elimu. Sasa jiulize ni elimu gani wanayotoa kwa staili hiyo.

    Tungelikuwa tunawachagua hawa watu kwa kura nadhani wasingelikuwapo kazini leo

    ReplyDelete
  7. Aibuuuu... yaani page kama ya mtoto anayejifunza kutengeneza website!

    ReplyDelete
  8. NASHUKURU KWA NAFASI MUHIMU SANA YA KUCHANGIA UPANDE HUU. ILA MIMI NAINGIA SAFU HII KULALAMIKIA CHUO KIKUU CHA TUMAINI DAR-ES-SALAAM. KWAKWELI ADA INAYOTOLEWA PALE NI KUBWA SANA' KWA HALI YA MTANZANIA WA KAWAIDA MILIONI MBILI NA LAKI TANO NI KIWANGO KIKUBWA SANA. PIA AFADHALI KIWANGO CHA ADA KITOLEWACHO KINGEKUWA KINAKIDHI HUDUMA, HAKUNA HOSTELS WANAFUNZ WANAPATA TABU KATIKA SUALA ZIMA LA MAKAZI VILE VILE LIBRARY HAKUNA VITABU MAGAZETI TU NDO YAMEJAA HUKO, COMPUTER LAB INA COMPUTERS CHACHE SANA NA KATIKA HIZO CHACHE WALA SI ZOTE ZIFANYAZO KAZI KWA UFASAHA HIVYO KUPELEA TABU KWA WANAFUNZI KATIKA KUJIFUNZA SOMO HILO. PIA HAKUNA VITI VYA KUTOSHA NA VYUMBA VYA KUSOMEA NI DOGO HIVY KUPELEKEA MADARASA MATATU TOFAUTI KUBADILISHANA CHUMBA KIMOJA AMBACHO NDO KIKUBWA PEKEE, KWA KWELI WANAFUNZI TUNAPATA SHIDA SANA NA UCHUNGU HASA PALE TUNAPO FIKIRIA KIASI CHA ADA WALICHOTOA WAZAZI WETU, KWELI INAUMIZA SANA, TAFADHALI SANA WADAU TUNAOMBA MSIMAMIE SUALA HILI KWANI MBONA WALE WA IRINGA HUDUMA ZAO NJEMA SANA?

    MDAU KATIKA ELIMU
    TUMAINI UNIVERSITY
    DAR-ES-SALAAM COLLEGE

    ReplyDelete
  9. Wow! kweli hiyo site ni kichekesho

    Mdau katika elimu ndio maana huku tuliko wnafanya open house. Ukiona shule inachemsha apply nyingine na uhamie huko. Naona vyo viko vingi sasa hivi bongo kwa hiyo kila mtu anauhuru wa kuchagua takacho. Ukiona sio kizuri unaaply kwngine ukikubaliwa unahama tu. Hela ya box tunaisotea sana hivyo ukienda shule unatafuta chuo unachoaaford lakini kiwe na hadhi.

    ReplyDelete
  10. Mdau wa Thu Nov 25, 06:52:00 PM kuhusu ada ya Tumaini University,naona maoni yako ni mazuri kama ukiyatuma kwa Bwana Michuzi ayaweke kama Post ili watu wachangie.

    Kukusaidia tu ,KAKA MICHUZI NAOMBA MAONI YA MDAU WA Thu Nov 25, 06:52:00 PM KUHUSU TUMAINI UNIVERSITY UYAWEKE KAMA POST

    ReplyDelete
  11. Afadhali wanajiita Shule (School) kwa kweli ni kama shule ya msingi ya kijijini tu! Huko kwenye website ni mbali sana ebu tembelea pale uone jengo chakavu limeongezwa ghorofa moja juu mpya! Kwanini wasingekarabati kwanza jengo chakavu lile? Ofisi mbovu, vyoo vibovu...

    ReplyDelete
  12. Japo mimi sio msemaji lakini napenda kuwafahamisha wadau kwamba website itakuwa tayari muda sio mrefu. Kwa sasa kuna website ya alumni wa UDSM School of Law (Formerly Faculty of Law) na wadau wanaweza kutembelea website hii: www.darlawalumni.ac.tz.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...