Waziri wa Habari,Utamaduni na Michezo,Mh. Dr. Emmanuel Nchimbi akiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi wa Benchmark Productions,Madame Ritha Paulsen katika ukumbi wa Mlimani City,jijini Dar zinakoendelea kufanyika fainali za BSS 2010 ambapo mshindi atakae patikana leo atajinyakulia kitita cha shilingi mil. 30 keshi.
Meneja wa Bia ya Kilimanjaro,George Kavishe akimuelezea jambo Waziri wa Habari,Utamaduni na Michezo,Mh. Emmanuel Nchimbi wakati wa hafla ya fainali za Bongo Star Search 2010 zinazoendelea kufanyika katika ukumbi wa Mlimani City,Jijini Dar usiku huu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 12 mpaka sasa

  1. hivi kaka michuzi inakuwaje kwenye shughuli nzito kama hii na wadau wa TBL wako around lakini ile kinywaji yetu toka aidha TBL au pale SBL haipo mezani. Mimi najua huu ni mwezi wa kilaji hasa kule kilimanjaro, ....kavishe ameniangusha

    ReplyDelete
  2. Acha ulevi wewe, siyo kila wakati wenzako wanawaza kilevi tu , kuna wakati wakujenga taifa pia! wewe mchaga gani !

    mdau china

    ReplyDelete
  3. JAMANI NIMEANGALIA HII SHOW JANA USIKU. KILICHO NISIKITISHA NI MASTER J KUTUKANA WATAZAMANI NA WAPIGAKURA KWA KUWAITA WASHAMBA KWA SABABU TU WALIMSHANGILIA MZUNGU NA KUMPIGIA KURA. SWALI LANGU, KWA NINI HUYO MZUNGU AKAWEPO KAMA HAKUTAKIWA KUPIGIWA KURA? NA KWANINI WAWACHAGULIE WATAZAMANIJI. SHOW ILITAWALIWA NA RACISM. MASTER J APOLOGIZE TO THE PUBLIC NA WAZIRI ALIYEKUWEPO.

    ReplyDelete
  4. Kitendo cha kuonyesha ubaguzi wa rangi kwenye BSS kimetusikitisha sana watanzania hasa pale master J kutuita watanzania washamba, sasa mashindano mmeweka yanini kama mnachagua wenyewe? Rita na master J acha hiyo !!

    ReplyDelete
  5. Bro Misup weka picha zaidi za bss na clip tuone hao majaji wasio na uzoefu na wala hawataki kujifunza kutokana na makosa yao.

    ReplyDelete
  6. nimeangalia BSS jana kilichokuwa kinaelezewa na master J pamoja na salama zidi ya mzungu 'JP' it was not crimes against individual or racism but it was crimes agaist humanity. na master j aliendeleza u-crimes wake kwa kumfananisha mshikaji na mfungua geti wake. it was a shame...

    to me this is the worsiest final since the establishment o BBS.


    JJB

    ReplyDelete
  7. Michuzi hebu tuwekee video yake tuione maana sisi wa mbali hatuelewi ilikuwaje na kwanini watu wamelalamikia sana show hiyo. tutashukuru kwa kufanya hivyo.
    mdau

    ReplyDelete
  8. Matokeo yamechakachuliwa. Mzungu hakustahili kuwa namba tatu. Ila nimempenda waliyeamua kumpa ushindi she was exceptional na alikomaa na taarabu mwanzo mpaka mwisho.

    ReplyDelete
  9. jana wamechakachua kabisa

    ReplyDelete
  10. jamani hiyo show bss michuzi ungetuwekea nasisi tulioko nje ya nchi tuweze kuona au kuna anayejua web site ya kuangalia bss live? pls kwa yeyote anayejua atujuze pls

    ReplyDelete
  11. wewe Mdau wa china...NIHAO, naombna nikupe taarifa kuwa kilaji ni sehemu ya maendeleo hapa Tanzania na si ulevi. Infakti beer is one of the most taxed item in the economy...and that means it contribute significantly to government revenue, employment to thousands of people in the economy, inatujumuisha wana jamii hasa wa huku mndenyi kilimanjaro..nk.nk.nk..if you drink responsbly no problem.

    ReplyDelete
  12. safi sana master j wewe kweli mzalendo. kwa sisi tulio ishi nje tuna kuelewa kabisa. wewe ndo mzalendo.watanzania wanafagiliaga ngozi nyeupe kiushamba , ..........
    mdau paris

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...