Mwimbaji Mtanzania anaetingisha kwa miondoko ya Bongo Fleva huko Uingereza, FRANCIA CHENGULA, ametoa Album yake mpya inayoitwa MOYO WANGU. Album hii kwa sasa inaweza kupatikana Itune, Napster and Amazon MP3. Kwa wale wanaotaka Hard Copy CD pia zinapatikana.

Nyimbo zote ni za Kiswahili na ni pamoja na ule wimbo Maridadi unaopendwa na uliovuma sana wa NAKUPENDA TANZANIA. WATU POPOTE DUNIANI WANAWEZA KUNUNUA KWA KUFUATA LINK HII HAPA

http://itunes.apple.com/us/album/moyo-wangu-ep/id410241720

Kwa maelezo zaidi au mawasiliano na team ya Francia
Piga simu no. 07789417307

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. Mbona kama nimesoma naye Oysterbay primary school, ni Francia John?

    ReplyDelete
  2. Ndio kasoma O'bay na makazi yao ni Regent estate area.

    hello na mie nimesoma nanyi mwaka mmoja mbele ya FranciaO'Bay primary.

    Oysterbay JUU oyeeeeee

    ReplyDelete
  3. Keep the flag flying girl, go go

    ReplyDelete
  4. Weka wimbo mmoja hapa michuzi, happened to hear a song in Tanzani, hongera sana dada

    ReplyDelete
  5. Kwa wenye credit cards, album ni bei nzuri tu 4.95$. Mi nimenunua sasa hivi. Lakini pia ni jukumu la msanii au wawakilishi wake kuhakikisha muziki unawekwa kwenye category sahihi ndani ya itunes, kwani huu muziki umekuwa listed kama "Gospel, Christian Music" -- kidogo tu nisinunue kama nisingesikiliza preview

    ReplyDelete
  6. Kweli Obay juu,kumbe niko sawa tulisoma wote , hongera sana Francia na nashukuru pia kunifahimsha juu yake mdau hapo.

    ReplyDelete
  7. Mi nilinunua sikua nimeangalia hiyo category. Ila nilisikiliza preview na nikazipenda nyimbo zote. Kwa huku Uk ni £3.95. Very nice songs hongera dada

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...