Nimegongana na hii video kule YouTube ikanikumbusha libeneke la waosha vinywa juu ya ung'eng'e wa kule Big Brother. Wadau wanaojua Kijapani, msaada tutani kama hii mistari imenyooka au ndo vile vile??

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 24 mpaka sasa

  1. Anajitahidi kwakweli, maana inaonyesha kakaa miaka 2 tu i guess mpaka hapo alipokuwa akiongea. Na pia kwa alivyojieleza kaoa mjapan. Kwa mtu ambaye si lugha yake yuko suppppaaaa!

    ReplyDelete
  2. Kijapani kajitahidi saaana, anastahili sifa na pongezi, ila wangemwambia aanze na nashibota, wakora na kuchanganya kidogo na kimombo angeenda speed zaidi

    ReplyDelete
  3. MWasi uko juu kaka.
    Mdau Uk

    ReplyDelete
  4. wewe ulioleta hii issue whats your point? unachotaka ni nini? Naona lengo lao lote ni umbea tu, Grow up!!!

    ReplyDelete
  5. Mwasi aminia sana, nimeipenda hii, Yaani bomba sana. Kamua mzee, haya mambo ndo tunahitaji, sio wabongo wanaenda nci za watu halafu wanapotea tu. Nimekukubali mzee.

    ReplyDelete
  6. Na mimi namshangaa sana aliyeleta hii post, anaonekana kama kakaa kidaku daku tu, ni ujinga, Kua kijana. Sio kukaa na kukosoa wenzako, sasa kama hujui alichoogea umeileta ya nini hapa. Wabongo mnafikiri Kiingereza tu ndo dili. Acheni ujinga.

    Mdau Netherlands.

    ReplyDelete
  7. KWA KWELI MWANA AMEJITAHIDI SANA KWA KIJAPAN, MAANA TUNA WENGINE HAPA MIAKA 15 HAWAWEZI KAMA HUYU BWANA MWASI ANAYOKIMWAGA KIJEPU ME NAMKUBALI SANA,SAFI MWANA. MDAU JAPENGA

    ReplyDelete
  8. BIG UP MKUU MWASI - MDAU UBATANI

    ReplyDelete
  9. Good job man!

    ReplyDelete
  10. HONGERA !!!Kuna watu kibao wamekaa hapa UK hata kakijisentensi kamoja ka english hawawezi kuandika,Kuongea ndo basi tena kazi yao kuwacheka wabongo walioko home kumbe wenyewe huku ni ZERO.
    Mdau wa UK

    ReplyDelete
  11. Mwasi,
    Babu kubwa Ndugu yangu.. lazima nii peleke kwa Mwalimu Gora pale Chang'ombe Shule ya Mazoezi apate kuuona vijana wake walivyo jitahidi kuishi vizuri na watu.

    ReplyDelete
  12. Ung'eng'e wa Big Brother unamaanisha Kanumba??
    Huyu kijana mbona anaongea vizuri tu hicho kijapani.
    Ongeza juhudi zaidi kakangu.. utakijua tu fasaha zaidi kama wao.

    ReplyDelete
  13. ...ahaa safiiiii..ebana nasubiria nije mwakani najua utanifunza sana kijepuuuu

    ReplyDelete
  14. Hata nami nashangazwa sana na mleta hii post hususan maneno aliyoyatumia inaonyesha dhahiri ni mdaku wa hali ya juu. Dhamira yake yote ya kuileta hii post ni kutaka watu hapa wamcheke huyo jamaa katika video lakini ime backfire!

    ReplyDelete
  15. Safi sana, inatakiwa Watanzania waliopo ughaibuni wajifunze lugha za wenyeji wao kwa bidii na kasi zaidi, ili tuweze kuitangaza Tanzania kwa lugha zote ikiwa pamoja na kuvutia ubia wa kiuchumi kupitia utalii, viwanda, usafirishaji n.k kupitia teknohama na hafla kama hii huko Japan.
    Mdau
    JeiKei

    ReplyDelete
  16. mdau alieleta post ni mjinga sana.yani unataka watu wakuambia kama jamaa anapatia wakati unaona wa japan wenyewe wanamuelewa?


    get a life.

    ReplyDelete
  17. aliyeleta hii post atakuwa anatafuta pa kuficha sura yake.hakuna hata aliyemsapoti na UDAKU wake.sidhaki kama ushawahi kuwacheka/dhihaki wageni wanaoishi bongo huku kiswahili kikiwasumbua.hao wanamuziki wa kikongo na nyimbo zao za kiswahili mbona zinafagiliwa ingawa lugha imepinda?
    Grow Up!!!!

    ReplyDelete
  18. cha msingi ni kwamba wenye lugha wanamuelewa, hiyo si lugha yake ya asili hivyo kinachotakiwa ni kueleweka tu

    ReplyDelete
  19. Sikielewi alichokuwa anasema jamaa huyu lakini kwa kutumia tu akili yangu inaonekana jamaa ni mkali kijapani anakijuwa si mmeona mpaka wenyewe wanacheka kwa kuwa wameelewa anachosema big up do wewe wa japan

    ReplyDelete
  20. amajitahidi, unajua hata wazungu wakija bongo hawaogopi kuchekwa ndio maana within a short period wanakua wameshajua kiswahili. kuogopa kukosea ndio kunaturudisha nyuma. tusipende kuchekana bali kupeana moyo

    ReplyDelete
  21. Kwa kweli sijui huyu kijana anaongea nini lakini hata kama anakosea kama mtuma post alivyoandika sioni cha ajabu. mi nafikiri ni kupungukiwa na mawazo kuanza kutafuta amechapia wapi...hakuna mtanzania aliyezaliwa akijua kijapan au kiingereza...wengi lugha hizi za kigeni ni za tatu au wengine ni za nne...sioni ajabu mtu akichapia. kwa kweli watanzania mnatia aibu...si ajabu hadi leo mkawa mnaongea lugha yenu ya taifa tu eti kwa kuogopa mtachapia...mawazo mgando kweli kweli...

    ReplyDelete
  22. Ningependa niangalie post hii kwa jicho la tatu. wengi tumemlaumu aliyeleta post hii na kumwita mdaku n.k Wote tumesahau mwenye kura ya turufu ya kuaomua ni post gani iende hewani ni Bw. Michuzi mwenyewe, kama post ni ya kijinga basi ilitakiwa isipate mpenyo kwenye blogu...kinyume chake, imepata. Nafikiri ni kulemaa kwa mkito wa fikra za Bw. Michuzi, kama post ni ya kipuuzi, inayorudisha juhudi za watanzania kujifunza jinsi ya kushiriki vyema kwenye utandawazi, basi na isiwekwe...kama ningekuwa natakiwa kuipa kura blogu hii kwa hii post, ningeipokonya kura moja...Bw. Michuzi, tafadhali onyesha frika zilizokomaa.

    ReplyDelete
  23. NIMESIKILIZA SIJAELEWA KITU

    ReplyDelete
  24. Kijana yuko juu ameongea vizuri mno, nimependa anavyozungusha vidole na mikono yake. waooo very nice.kwanza mcheki anavyopresent anavyoweka mikono na vidole vyake, anapendeza kweli.Pili anajiamini na anachokiongea watu wanamuitikia vizuri hawaguni.nimependa sana .Uncle asante kwa changamoto hii uliyotuletea wengine tujifunze,kupanuka kifikra na mtazamo. Kujifunza lugha za watu popote pale hata ukipostiwa kwenda umakondeni kikazi jitahidini kujifunza japo maneno wawili matatu. Nimepostiwa Dodoma lol.. kikazi walau najua maneno mawili matatu hivi ya KIGOGO.tehetehteht....

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...