Hivi ndivyo soko la Mbeya uhindini linavyo onekana kwa sasa. Kwa hakika walio kuwa na maduka makubwa wote wameathirika kwa kiasi kikubwa sana na janga hilo la moto. Maduka makubwa sokoni hapo likiwemo la Mushi na Nanetelecomunnication yanayo angalia upande wa Benki ya NMB Mbalizi Road hayakuambulia kitu chochote kutokana na Moto kuunguza kila kitu na kuzingira eneo lote hilo...Taarifa zaidi zitazidi kuwajia.
Picha na Ripota wa Globu ya Jamii, Mbeya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. kwanza poleni sana watu wote walioathirika na moto huu. Pili nadhani huu ni wakati muafaka wa kufikiria bima za moto kwa wafanya biashara wadogo wadogo.

    ReplyDelete
  2. Tupe Tamko la Mbunge wa huko kuhusiana na hali hiyo tafadhali!

    ReplyDelete
  3. Hadj Drogba "mwana chelsea"December 02, 2010

    Pole sana Mh.JOSEPH MBILINYI kwa watu wako wapendwa kuunguliwa na maduka yao,ama kwa hakika hiyo ni changamoto ya kwanza kwako.Pia hiyo sehemu iliyotajwa kuteketea kabisa lipo duka la dadangu schoolmate wangu sangu secondary 1990-1994 Agnes Memba popote alipo nampa pole yeye na mdogo wake,ni watu wazuri sana

    ReplyDelete
  4. Mbona Jiji la Mbeya laandamwa na majanga ya kuungua kwa masoko yake?

    ReplyDelete
  5. Mbeya kunani tena?

    Mwaka ulee ilikuwa Mwanjelwa moto mpaka chini. Leo ni Uhindini.

    Mbona masoko ya huko yanapotea kwa moto tu? Halafu utasikia baada ya moto hakuna tena watu kurudi hapo bali watahamishiwa eneo jingine.

    Somethingy smells fishy here!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...