Hi Ankal,
Pole sana na jukumu zima la kutupasha habari za nyumbani. Hakika mdau wa Ukweli hapa na kuna mdau kutoka Urusi kanitumia hii picha kwenye akaunti ya Uso wa Kitabu na mie nikaona isiwe uchoyo tukichanga!

Aniwies hapaa inaonesha kwa jinsi gani darasani wanafunzi wake walikuwa wanafanya sana "cheating" kwa kuchunguliana na ndio wakabuni njia mpya ya JIBEBE MWENYEWE. Hahahahaha! Hahahahaha! Yaani huyu mwalimu alifanya jambo sahihi kwa kuanzisha njia hii.

Itakuwa vipi kama Mh. Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi akiliona hili na kulichukulia hatua kwa Elimu ya Bongo!!! Naona ugumu utazidi mara dufu! Maana duuuuh! Sipati tutafaulu wangapi miongoni mwetu! Maana kuna wale watu tunapepesa sana macho kama indiketa ya ISUZU...!!!

Ahsante sana na nakutakia kazi njema!
Mdau kutoka Solvesborg, Sweden.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. huu ni uongo,urusi kuna Tech ya kutosha zaidi ya gamba la jarida. Kama ni kweli basi ni bongo.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...