Natumai bwana Ankal na wadau wa Globu ya Jamii m wazima? Hapa nimeona nishee na wakereketwa wengine mambo mazuri ya kukumbukwa. Nilifanikiwa kupata picha ya S.S.C a.k.a Lunyasi wakati huo.Hii ilikuwa 1990 na pamoja kufuatilia kwangu soccer sina kumbukumbu ya majina yote. Je kuna watu wanweza kutatua utata ? Ni nani majina ya wachezaji waliopo katika picha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. duh, kipa ni mwameja, kushoto yake ni george masatu, wajuu yake ni hussen masha, wa tatu kutoka kushoto kwa ktk ni gebo peter, NAWAKUMBUKA HAO TU NA PIA SINA UHAKIKA.

    ReplyDelete
  2. huwa sipendi kukosoa sana watu lakini napenda kuweka kumbukubu sawa hii sio simba ya mwaka 1990 itakuwa ya kuanzia mwaka 1992 au 1993.kwa kuwa 1990 simba walikuwa na mastaa hawa HAMIS THOBIAS GAGARINO,ZAMOYONI MOGELLA,MEKENZIE RAMADHANI,MAVUMBI OMAR,DEO NJOHOLE OCD,METHOD MOGELLA,EDWARD CHUMILA,ALLY YUSUPH CHABALLA,TWAHA HAMIDU,NA YA 1991 ONGEZA KASANGA BWALYA,IDD PAZI, ITUTU KIGI,HASSAN AFIFU,JAMHURI KIWELU MREMA,KHALFAN NGASA,AYUBU MZEE,SASA HAPO NAWAONA AKINA MWAMRJA AMBAE ALIKUJA 1992,DAMIEN MRISHO KIMTI,MASHA,GEBO PETER,KASONGO ATHUMANI.NK.


    OCD

    ReplyDelete
  3. DUUUUUU!...hiki ni kikosi kilichotwaa ubingwa wa afrika mashariki mara mbili....,hapo juu ni bila kumsahau MALOTA SOMA "Ball Jugler",Madaraka Selemani" mzee wa kiminyio", nduguye IDDI SELEMANI,TWAHA HAMIDU,RAPHAEL PAUL"the road patrol",...kikosi hicho kamisi Ramadhani Leny..aliyefariki kipindi cha miaka ya 94...,Gagarino ndio alikuwa ameanza kudrop..hasa kutokana na kinywaji...ndo maana mnamuona Huseein Marsha hapo....aliyesajiliwa haraka kuziba pengo la GAGA na method mogella aliziba pengo la Japo hakukaa sana...kulikuwa na dogo mmoja aliyekuwa akiitwa HUSSEIN MACHELA...hapo..na ndio kipindi pia JOHN MAKELE alikuwa anamalizia malizia makali yake..!

    Hapo mfadhili mkuu alikuwa AZIM DEWJI,akisaidiwa na kina AHEMD BORA...nduguye SHAFIE BORA wa majimaji....[hapo inafanya nimkumbuke na KAKA wa TUKUYU STARS]...,...MRATIBU wa timu alikuwa JABIR ALI SHIKAMKONO.....na super chairman..SHEIKH AMIRI ALI "bamchawi"...makamu ..mzee GHULLUM..,na kina FAKHRUDIN AMIJEE...

    Octavian Mshiu.

    ReplyDelete
  4. braza mbona yanga huwaweki hata picha moja

    ReplyDelete
  5. Kweli OCD,hii itakuwa baaada ya 1990,kwani kama ulivyotaja akina Hussein Marsha na Masatu walikuwa Pamba mwaka huo.

    ReplyDelete
  6. NYUMA-idd pazi,issa kihange,fikiri magoso,george lucas nyeo*GAZA*,idd selemen,ally machella,
    KATI-gebo peter,michael paul,husein masha,alfred kategile,hamza maneno
    MBELE-deo njohole,joseph lubisha,damian kimti,moh mwameja,kasongo athuman,twaha hamidu.ZANZIBAR AMAAN STADIUM 1992

    MASIMBA

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...