Marehemu Aisha Famau (Aida)

Familia ya Mzee Emily (Nembo) inawatangazia kifo cha mtoto wao na ndugu yao mpendwa Aisha Famau (Aida) kilichotokea tarehe 03/02/2011 nyumbani kwa marehemu Leicester (UK).

Mazishi yatafanyika JUMATATU 21/02/2011.

Nafasi ya kutoa heshima za mwisho kwa marehemu itaanza Saa tatu asubuhi hadi Saa Nne asubuhi kwenye anwani ifuatayo:

Co-operative Funeral Services,

131 Humberstone Road, Leicester, LE5 3AD

Baada ya hapo utafuata msafara wa kupeleka mwili wa marehemu kanisani, msafara huo utapitia St Mattehws eneo alilokuwa akiishi marehemu.

Ibada ya mazishi itaanza saa nne na nusu asubuhi katika kanisa la

Sacred Heart Church, 25 Mere Road, Leicester, LE5 3HS.

Baada ya ibada mwili wa marehemu utapelekwa kwenye makaburi ya Gilroes Cementry ,

Groby Road Leicester, LE 3 9QG – saa sita mchana kwa mazishi

Baada ya shughuli za mazishi kumalizika kutakuwa na chakula cha mchana kwenye ukumbi wa kanisa ilikofanyikia ibada

Kwa ushirikiano wetu wa dhati tutafanikisha safari hii ya mwisho ya mpendwa wetu.

Usafiri utakuwepo kwa wale wasiokuwa na usafiri

BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA, JINA LA BWANA LIHIMIDIWE MILELE.

MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI.

AMINA

Kwa maelezo zaidi wasiliana na :

Asela: 07932841352

Abdullah: 0791957846

Moses: 07405272879

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Poleni sana wafiwa. Mwenyezi Mungu awajaze faraja na kuipokea roho ya marehemu mbinguni.

    Mdau
    London

    ReplyDelete
  2. I deeply saddened to hear the loss of Dear Sister Aida. May she Rest in Eternal Peace. Amen.

    ReplyDelete
  3. Poleni sana ndugu zangu jamani, ni machungu mazito yasiyoelezeka kwa kumpoteza ndugu yetu,rafiki yetu na mpendwa wetu Aida,Mungu awatie nguvu na awape faraja ya pekee katika kipindi hiki kigumu.Sisi tulimpenda lakini Mungu amempenda zaidi basi tumuombee apumzike kwa amani.Faraja ya pekee iwaendee hasa watoto wake na mume wake.
    R.I.P Aida pumzika kwa amani mama.

    Rafiki wa rafiki zake
    London

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...