Marehemu Mzee Luanda (kwenye kiti) mwanae mkubwa Beda Msimbe (kulia), na wadogo zake Beda pamoja na kaka binadamu Lubuko katika picha ambayo mwenyewe akiwa hospitalini alisema njoo nipige picha.walichekeshana kidogo, bila kujua kwamba hiyo ndiyo picha ya mwisho naye.

Mtangazaji wa zamani wa Radio Tanzania John Luwanda amefariki dunia Muhimbili leo mchana baada ya kuugua kwa siku kadhaa.

Mtangazaji huyo wa zamani ambaye alistaafu kazi hiyo mwanzoni mwa miaka ya 1990 alikuwa amelazwa hospitali ya Muhimbili akisumbuliwa na kisukari huku akifanyiwa uchunguzi wakansa ya kibofu cha mkojo.

Madaktari walimwambia kwamba baba yake alikufa kutokana na ugonjwa wa uti wa mgongo.

Mzee Luwanda ambaye atakumbukwa zaidi na watu wa vikundi vya sanaa kwa uandalizi wa michezo ya kuigiza ya radio, mara baada ya kustaafu alikuwa anaishi katika kijiji cha Goba akilima bustani na kufuga.

Mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwake Gobakijijini na anatarajiwa kuzikwa Jumamosi wiki hii.Luwanda ameacha mke watoto 6 na wajukuu 20.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. RIP John Luanda.....

    ReplyDelete
  2. Mungu amlaze mahali pema Peponi Mzee Luanda.

    ReplyDelete
  3. Mungu amlaze pema mzee Luanda

    ReplyDelete
  4. RIP MZEE JOHN LUANDA. POLENI SANA FAMILIA, NDUGU JAMAA NA MARAFIKI KWA MSIBA HUU MZITO.
    MDAU

    ReplyDelete
  5. Rest in Peace Mzee Luanda. Pole sana Kaka Beda na wanafamilia. Ingekuwa vizuri kama RTD wangefanya kipindi maalum cha kumkumbuka.

    ReplyDelete
  6. RIP mzee wetu. Pole sana sana Beda, ndugu, jamaa na wanafamilia wote. Tulimpenda mzee lakini Mola amempenda zaidi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...