
Nyumba iliyozinduliwa inagharimu Milioni 25 za Tanzania na inaweza kupanda kutegemea na mahitaji ya mteja mwenyewe anataka nini kiongezeke katika kuboresha zaidi nyumba yake, Lakini pia nyumba hizo zimebuniwa ili kusaidia watu wenye kupato cha kawaida ambao kwa upande wao kujenga inakuwa ni kazi ngumu hivyo kupitia mradi huu wa Nyumba Poa Model House watu wa kipato cha chini wanaweza kujipatia nyumba bila matatizo
Akizungumza katika uzinduzi huo Mh. Bernald Membe ameishukuru kampuni ya Nyumba Poa LTD kwa kuanzisha mradi huo hapa nyumbani kwani wameamua kuitikia wito wa serikali na kuja kuwekeza nyumbani, amesema Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete pamoja na yeye mwenye wamekuwa wakiwaasa Watanzania wengi walioko nje ya nchi kurudi nyumbani na kuwekeza au kuwekeza nyumbani wakiwa hukohuko nje jambo ambalo Kampuni ya Nyumba Poa LTD imeitikia kwa vitendo.
Wanaoshuhudia ukataji wa utepe kutoka kulia ni Daniel Mziray Mkurugenzi wa ufundi wa Kampuni ya Nyumba Poa LTD na Peter Malika Mkurugenzi wa Kampuni hiyo.
Kwa Hotuba kamili ya Mh Membe
BOFYA HAPA.




na uraia wa nchi mbili je?
ReplyDeleteTupatie contact address zenu maana hizo ndiyo nyumba type yetu sisi wafanyakazi wa Serikali.
ReplyDeleteMikopo benki haichukuliki kwa riba tunatarajia nyinyi mutakuwa na makubaliano yaliyo na unafuu.
hii ni safi sana. watanzania mlioko nje endeleeni kuwekeza nyumbani.
ReplyDeletemsisahau kilimo na mambo mengine. serikali inatakiwa kuwapa kipaumbele
watanzanio walioko nje na ndani ya nchi kuwekeza tanzania. serikali isipendelee matapeli kutoka nje.
Hongera sana ndugu Peter Malika kwa maamuzi uliochukua ya kuwekeza katika nchi yako ya Tanzania,pia hongera kwa kuleta maendeleo katika jamii yako kwa ujumla na watanzania wote,Mungu akubariki sana na kukupa akili ya kugundua uwekezaji mwingine zaidi ya huu kwa ajili ya maendeleo ya taifa kwa ujumla..
ReplyDeletePia napenda kutoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh jakaya Mrisho Kikwete kwa kutoa changamoto zidi ya Watanzania waishio nchi za nje kuja na kuekeza nchini mwao,pia shukrani zingine zimwendee Waziri wa nchi za nje Mh Benard Membe kwa kauli nzuri ya kuwatia moyo Watanzania wanaotaka kuwekeza nchini mwao..
Mungu akubariki sana Peter Malika katika uwekezaji wako.