Nakuchukua nafasi hii kutoa shukrani zangu za dhati na za kipekee kwa wafanyakazi wenzangu wote na uongozi mzima wa chuo cha usimamizi wa fedha (IFM) kwa kunisupport na kunifariji katika kipindi hiki kigumu cha msiba mzito wa mama yangu mpendwa Asha Nassibu Shefa kilichotokea tarehe 7 March 2011. Inshallah MwenyeziMungu atawalipa kwa hilo.

Pia napenda kuwashukuru wafanyakazi wa mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) ambapo marehemu ndio alipokuwa anafanya kazi wakati wa uhai wake. Pia nawashukuru wafanyakazi wa Mamlaka ya viwanja vya ndege(TAA) kwa msaada wao wa hali na mali.

Pia nawashukuru sana watanzania wote waishio stochkhom(Sweden) kwa kuandaa na kusoma kisomo cha kumuombea mama yetu mpendwa kilichofanyika tar 19 mwezi huu huko Sweden.

Nawashukuru marafiki zangu wote wa hapa nyumbani Tanzania pamoja na marafiki zangu waishio uingereza na wengine wote popote pale walipo. Bila ya kuwasahau majirani zangu.Nawashukuru sana.

ASANTENI SANA NYOTE, NA MUNGU AWABARIKI

Fatma Shefa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Poleni sana Fatma, Mungu azidi kuwatia nguvu.

    ReplyDelete
  2. Lydia KamwagaMarch 23, 2011

    Pole sana Fatma, sisi tulimpenda lakini Mungu alimpenda zaidi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...