Hi Ankal Michuzi!!
 
Napenda kutoa shukuran zangu za dhati klwa globu hii ya jamii kwa msaada mlionipatia,  Siku ya jumamosi mchana saa saba mwanangu Zuhura Mgweno alinipigia simu na kusema aliambiwa na mwanae kuwa natafutwa na mama yangu kupita blog hii.

Zuhura anasema alipoteza mawasiliano ndio sababu ya ukimya huo,kusema haki nilifurahi kupita kiasi na hapa nilipo nina furaha isiyo kifani jamani,sina la kusema zaidi ya kusema asanteni sana kwako wewe Issa Michuzi na waliotoa maoni wote kwa msaada wenu.

Sina cha kuwalipa zaidi ya kuwaombea furaha na amani katika maisha yenu.
 
 Akhsante Mdau

Habari kamili za Mama kumtafuta Da'Zuhura

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 20, 2011

    Ankal Michu japo simjui huyu dada, nilposoma habari hii nimefurahi mpaka kidogo machozi yanitoke kwa kuzingatia hisia mama yake alizopitia. Fatma wa Chang'ombe, DSM.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 20, 2011

    Safi sana. Ndiyo maana blog hii ni blogspot ya kwanza katika blogspots zote za TZ kwa kuhudhuriwa (visitors' traffic). Keep it up bro. Mdau wa utafiti wa Information Superhighway Traffic in Africa. (USA).

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 20, 2011

    EMOTION..mwili umenisisimka sana jamani kiasi nilie,ankali mungu akupe umri mrefu wenye afya tele ili uweza kuendelea kuisaidia jamii..

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 20, 2011

    Tunashukuru GLOBU ya JAMII kwa kutumikia JAMII

    ReplyDelete
  5. Hii BULOGI ya MISUPU inasaidia sana jamani!

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 20, 2011

    JAMANI NIMEFURAHI SANA KAMA ZUHURA AMEWEZA KUWASILIANA NA MAMA YAKE..ZUHURA TUNAKUOMBA USIKAE SANA KIMYA UNAWAPA SHIDA WAZAZI..NIMEFURAHI SANA..BLOG YA JAMII OYEEEEEE

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 20, 2011

    Michuzi,

    Nilikutumia ujumbe asubuhi kutaka kurekebishwa kwa habari hii. Hii habari ina upotoshaji ndani yake. Katika ujumbe niliokutumia asubuhi nilimuomba huyu Shangazi ajitokeze kurekebisha ujumbe wake.

    Zuhura ambaye habari hizi zinapotoshwa juu yake hana uwezo wa kujitetea hapa kwa kuwa ni mlemavu wa kusikia na kuongea.

    Huyo anayedai ni Mama yake Zuhura siyo kweli ni Mama yake Zuhura. Zuhura anaishi na Binti yake na Mama yake mzazi mjini Oulu, Finland. Huyu anayejiita Mama yake Zuhura ni shangazi yake Zuhura na wala siyo Mama yake kama anavyodai.

    Laiti kama ungemjua Zuhura ambaye huyu Shangazi anamchafua jina sidhani kama ungeacha kuweka maoni niliyokutumia asubuhi.

    Nakuomba utende haki kwa kuweka ujumbe niliokutumia asubuhi pamoja na huu ninaokutumia jioni hii.

    Asante sana.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 20, 2011

    Mpaka ukitafuta kwenye mablogg uwasiliane na mama yako aliyekuzaa. Katika dunia ya leo yenye mawasiliano ya kisasa ambayo yako bwerere huniambii kitu you are either insane or out of your mind!!!! Lakini pia nitatoa shukrani kwa blogg.
    MSEMAKWELI

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 21, 2011

    mungu akubari michuzi japo simwelewi huyo mama na huyo dada lakini nimefurahi sana kusikia amepatikana kupitia blog yako michuzi mungu akubariki sana na kazi yako na nakuombea maisha marefu yenye mafanikio mema najua kupitia glob yako wengi wanafanikiwa n matatizo yao god bless

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...