Dr Mukwege na tuzo yake
Mahojiano maalumu na Dr Denis Mukwege mwanzilishi na mkuu wa hospitali ya Panzi iliyoko Bukavu jimboni Kivu Mashariki mwa Jamhuri ya Kimokrasia ya Congo. 


Dr Mukwege ameshinda tuzo ya kimataifa kutoka ufalme wa Ubeligiji kwa mchango wake wa kusaidia jamii. Hospitali ya Panzi inahusika na kuwapokea, kuwatibu, kuwapa ushauri nasaha, kuwasaidia na kuwawezesha wanawake waliobakwa Jamhuri ya Kimokrasia ya Congo na inaungwa mkono na Umoja wa Mataifa, Jumuiya ya Kimataifa, mashirika yasiyo ya kiserikali na wahisani mbalimbali wanaopinga ukatili dhidi ya wanawake na hasa ubakaji. 


Amezungumza na mwandishi wa kujitolea wa Umoja wa Mataifa mjini Bukavu Mseke Dide kuhusu tuzo hiyo iliyoambatana na kitita cha fedha dola za Kimarekani zaidi ya laki mbili, kuhudu tuzo yenyewe, anachokifanya hospitali ya Panzi na malengo yake ya baadaye. 

Kusikiliza mahojiano haya bofya

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...