![]() |
Mcheza shoo Mkongwe nchini,Aisha Madinda. |
Na Mwandishi Wetu.
MCHEZA shoo mkongwe na maarufu wa Bendi ya Muziki wa dansi ya Twanga Pepeta, Aisha Madinda leo amejiunga rasmi na Bendi ya jirani ya Extra Bongo.
Akimtambulisha kwa waandishi wa habari,Mkurugenzi wa Extra Bongo, Ally Chocky alisema anafuraha sana kumpata mcheza shoo ambaye anamini ataleta mabadiliko ndani ya Extra Bongo kulingana na uwezo wake na jinsi anavyomfahamu.
Akizungumza na waandishi wa habari,Aisha Madinda amesema ameamua kuungana na wacheza shoo ambao anaamini akiwa nao katika safu hiyo atafanya vizuri na kipaji chake kitazidi kupanda juu zaidi.
![]() |
Mkurugenzi wa Bendi ya Exta Bongo,Ally Choki akimtambulisha Aisha Madinda leo |
Aisha tayari ameshaanza mazoezi na atatambulishwa rasmi kwa mashabiki jumatno kwenye Klabu ya masai Ilala jijini Dar es Salaam
Kiongozi wa wacheza Shoo, Super Nyamwela alimkaribisha Aisha kwa mikono miwili na kusema sasa kazi imekamilika na kuwataka wapenzi na mashabiki wajitokeze kwa wingi mara ya kwanza wanapomtambulisha Aisha pale klabu masai Ilala ndipo moto mkali wa Exra Bongo utaanza kuwaka
ZE FULANAZ ILIPIGWA PHOTOCOY NINI NA ALLY CHOKI NDIO IMETOKA RANGI HIYO EH?????? SI ILE YA SKY BLUE NA WEUPE??? YA ANKAL MICHUZI.
ReplyDeletemi naona kesha kuwa mtu mzima shughuli haziwezi tena, ni bora angekaa nyumbani tu akawachia vijana sasa
ReplyDelete