Foleni barabara ya Kilwa road jijini Dar. Sijui kifanyike nini ili kukata hiki kimeo...

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 04, 2011

    Kwani nani kawaambia ku-control foleni inahitaji Rocket Scientist? hiyo ni kazi ndogo sana kama viongozi wako tayari kutumia brains zao. Nchi nyingi duniani zimeshafanikiwa ku-control foleni ikiwa ni pamoja na kupanua miji: Uncle labda mimi nitoe ushauri huu:
    1. Iwe marufuku kuendelea kujenga katikati ya mji majengo marefu na kufungua maofisi makubwa...mji unatakiwa upanuke kuanzishwe vitongoji vingine ili huduma muhimu zipatikane sehemu tofauti.
    2. Decentralization ni muhimu sana Tanzania. Kuna haja gani ya mtu kusafiri toka Arusha kwenda kwenye huduma ya kiserikali Dar? Kwanini kusifunguliwe ofisi mikoani ambazo zinatoa full service kwa niaba ya wizara na taasisi mbali mbali? Kwani tofauti iko wapi? Kama kuna maofisa wa Ardhi makao makuu Dar, kwanini baadhi yao wasihamishiwe mikoani wakatoa hizo huduma huko ili kupunguza mlundikano wa watu Dar?
    3. Kuanzishwe lanes za mabasi. Kukianzishwa high speed lanes za mabasi watu wataona ni nafuu kupanda mabasi na wataacha magari yao nyumbani kwavile mabasi yatakuwa na haraka zaidi. Halafu dala dala ndogo ziondolewe pawekwe mabasi makubwa.
    4. Wekeni nondo barabarani kuepuka watu kuvunja sheria. Barabara ziwekwe nondo (milingoti mifupi tu) ili magari yasiwe na uwezo wa kukatiza na kuvunja sheria.

    Kama mnahitaji ushauri zaidi wasilianeni na mimi hapa hapa...!!

    Tumechoookaaaaa....! Mdau-USA

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 04, 2011

    Wengi wetu hatujui kifanyike nini lakini nchi yetu imebahatika kuongozwa na wasomi. Rais ni Dr., Makamu wa Rais ni Dr., Waziri wa Ardhi na Makazi ni Dr., Waziri wa Elimu ni Dr., Waziri wa Maendeleo ya Mifugo ni Dr., Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknoljia ni Dr., Waziri wa Kilimo Chakula na Vyama vya Ushirika ni Dr. (Prof), Wazari wa Maji ni Dr. (Prof), Waziri wa Viwanda na Biashara ni Dr., Waziri wa Habari Utamaduni Michezo na Vijana ni Dr.,Waziri wa Ujenzi ni Dr., Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira ni Dr., Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji ni Dr.,

    Mimi ni matumaini yangu kuwa madokta wote hao wenye mamlaka kwa pamoja wanajua nini kifanyike. Swali ninalojiuliza mimi ni kwanini hawafanyi hicho kinachotakiwa kufanyika. Vinginevyo kama pamoja na usomi na mamlaka nao hawajui kifanyike nini basi shughuli ipo tena pevu!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 04, 2011

    Kaka michuzi. Hapa kuna tatizo kwa sababu ya namna ya kuingia mjini. Kama ningelikwua Rais wa nchi hii, ningeamuru kutengeneza flaiova kuanzia pale benderatatu kwenda posta kuingilia pale Water front chwaaaaa kwa wale wa posta halafu wale wa kariakoo watajiendeleza.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 04, 2011

    Jambo, kwa barabara ya kilwa road, kuna vivuko viwili (1) kama unaelekea mjini town pale BP relini ni kikwazo ile flaiova itafaa hapa, (2) kama ni kuelekea mbagala, kikwazo ni zile bwawa za samaki pale mbagala, ikigeuzwa kuwa barabara barabara ya kilwa road ni ........very very
    hebu cheki kama saba saba ground imefunguliwa hapo ni ishu pia.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 04, 2011

    MICHUZI HYO CO BARABARA YA KILWA ROAD KAMA PCHA INAVYOONYESHA
    BALI N CHAN'GOMBE ROAD
    INGAWA ATA KILWA ROAD NAYO PIA INA FOLEN

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...