Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk.Hussein Mwinyi akizindua Kitabu cha dini cha Mwezi Upi Sahihi wa ‘Kitaifa’ au wa ‘Kimataifa’. Kushoto ni mtunzi wa Kitabu hicho, Sheikh Profesa Mikidadi Juma na Mwenyekiti wa jopo la masheikh na wanazuoni wa Kiislamu Tanzania, Sheikh Sharif Hassan Hashim. Hafla hiyo imefanyika leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk.Hussein Mwinyi akizungumza wakati wa uzindua wa Kitabu cha dini cha Mwezi Upi Sahihi wa ‘Kitaifa’ au wa ‘Kimataifa’. Kushoto ni mtunzi wa Kitabu hicho, Sheikh Mikidadi Juma na wa pili kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa jopo la masheikh na wanazuoni wa Kiislamu Tanzania, Sheikh Sharif Hassan Hashim. Hafla hiyo imefanyika leo jijini Dar es Salaam.
Bango la uzinduzi
Mawaidha yakitolewa wakati wa uzinduzi huo
Sehemu ya waliohudhuria hafla hiyo adhimu. Picha na Francis Dande wa Globu ya Jamii
Mwezi Mtukufu wa Ramadhani hauko mbali, Mwenyezi Mungu ajaalie tofauti za kuanza kufunga na kufungua zisitokee tena.
ReplyDeletehii jumuia si ingelikuwa murua zaidi kama ingelikuwa na jina la kiswahili na kiarabu badala ya kiswahili na kiingilishi? Hasa ukitilia maanani ni jumuia ya kiislamu na lugha kuu pamoja na maamrisho ya dini hii yako katika kiarabu?
ReplyDeleteHivi kuna miezi mingapi? hili kwangu naona linawachanganya waumini, ingetakiwa maulamaa, wake pamoja wakubaliane, na waondoe tofauti zao, au wawaweke waumini sawa, kuwakutokana na hili na lile ni hiayari yako sasa kufuata huu au ule, kama ipo hivyo!
ReplyDeleteUtandawazi umekua, na hii ni sehemu ya changamoto inayokabili Waislamu katika masuala mfano wa haya. Leo hii mtu akitazama channel za Uarabuni mfano wa Saudia au Peace TV, anaona watu wakiswali swala mathalan taraaweh katika wakati ule ule na tarehe ile ile ya hapa kwetu. Utamlaumu mtu kwa hili, hasa ukizingatia kuwa mwezi ni mmoja tu duniani?
ReplyDeletenahitaji hiki kitabu mwenye kujua namna ya kukipata
ReplyDelete