Mabondia Mbwana Matumla (kushoto) na Francis Miyeyusho wakishikana mikono baada ya kusaini mkataba wa pambano kati yao, Dar es Salaam jana, mbele ya Mwanasheria Yasini Membar (wa tatu kushoto) wa Kampuni ya Mawakili ya Membar Law Attorney, Rais wa Shirikisho la Masumbwi Tanzania (PST), Emmanuel Mlundwa (kushoto) na Mkurugenzi wa Kampuni ya Dar World Link, Moddy Bawazir, ambao ni waandaaji wa pambano hilo.
Bondia Francis Miyeyusho akisaini hati ya makubaliano ya mpambano, Dar es Salaam jana kati yake na Mbwana Matumla 'Golden Boy' (kushoto), katika mtanange utakaofanyika Oktoba 30, ukumbi wa Diamond Jubilee. Anayeangalia ni Mwanasheria Yasin Membar wa Kampuni ya Mawakili ya Membar Law Attorney na waliosimama nyuma ni Mkurugenzi wa Dar World Link, Moddy Bawazir (kushoto), ambao ni waandaaji wa pambano hilo na Emmanuel Mlundwa, Rais wa Shirikisho la Masumbwi Tanzania (PST).
Bondia Mbwana Matumla, akisaini hati ya makubaliano ya mpambano, Dar es Salaam jana kati yake na Francis Miyeyusho (kulia) katika mtanange utakaofanyika Oktoba 30, ukumbi wa Diamond Jubilee. Anayeangalia ni Mwanasheria Yasin Membar wa Kampuni ya Mawakili ya Membar Law Attorney na aliyesimama nyuma niMkurugenzi wa Dar World Link, Moddy Bawazir, ambao ni waandaaji wa pambano hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 18, 2011

    Nataka huyo miyeyusho ambonde huyo matumla hadi basi Mungu msaidie miyeyosho ashide, Amen!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...