Wakongwe wakirekodi vibao vyao Metro Studios kwa Allan Mapigo
Kanku Kelly, Mafumu Bilali na King Maluu
Timu ya wakongwe wa muziki wa dansi nchini inayowakusanya wanamuziki akiwemo King Kikii, Mafumu Bilali, Bombenga Kasongo Mpinda, John Kitime, Abdul Salvador, Babu Njenje, Waziri Ally, Kanku Kelly, King Maluu, Andy Swebe,  Juma Ubao na wengineo, wanatarajia kufanya tamasha lao ambalo hufanyika kila mwaka na safari hii liko njiani kuelekea kileleni kwani linatarajiwa kufanyika kwenye ukumbi wa  Selander Bridge Club, maeneo ya Upanga  jijini Dar,  leo Ijumaa  tarehe 22 Julai 2011.

Lengo la tamasha hilo ni kuhuisha uwepo wa wanamuziki wa zamani kwa kudhihirisha kuwa uwezo wao kisanii bado uko juu, halikadhalika mchango wao katika kudumisha sanaa ya muziki wa Tanzania upo pale pale na pia kuikumbusha jamii kuwa walikuwepo, wapo na wataendelea kuwepo.

Nia yao nyingine, ni kuweka daraja baina ya wanamuziki wakongwe na wasasa ili kutengeneza muendelezo mzuri unaotokea kwenye chimbuko la muziki wa kitanzania na kuwaonesha vijana wanaochipukia kisanii kuwa muziki umetoka wapi, unaenda wapi na umefika wapi.

Abdul salvador, Waziri Ally na John Kitime
Siku hiyo inatarijiwa kuwa ni siku ya aina yake kwani wakongwe hao wanatarajia kutambulisha wimbo wao mmoja na mpya kati ya nyimbo tatu walizorekodi, na wimbo huo unajulikana kwa jina la Tanzania, wakiwa wame urudia katika midundo ya kisasa,kwani wenyewe ulipigwa na Atomic Jazz Band chini ya utunzi wake Steven Hiza mnamo mwaka 1965.

Wakongwe hao wameshakamilisha nyimbo zao tatu ikiwepo hiyo Tanzania, Miaka Hamsini ya uhuru pamoja na Kilimo kwanza na zote hizo chini ya usimamizi wake Prodyuza Allan Mapigo wa Metro Studio.

Kwa kuwapa Saport wakongwe hao ni kuchangia kwa kiasi kikubwa kuuinua muziki wa watanzania.


Wote Mnakaribishwa

 Wakongwe Juma Ubao na Andy Swebe mazoezini


 Kasongo Mpinda na King Kikiii
Marashi ya Karafuu...

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Mbona hamjasema kiingilio itakuwa sh ngapi,,na shoo itaanza sa ngapi?


    Mdau

    Dr Ray

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...