Wiki kadhaa zilizopita tuliwaletea picha mbalimbali kutoka katika location mbalimbali wakati wa kutengeneza video ya wimbo Kama Ipo(Kupanda na Kushuka) kutoka kwa msanii mkongwe kabisa katika Hip Hop nchini Tanzania,Professor Jay au ukipenda unaweza kumwita kwa jina lake halisi,Joseph Haule aka The Heavy Weight MC.

Matokeo ya kazi ile ni haya hapa; Ni video nyingine kutoka Visual Lab.Kama lilivyo jina la wimbo,kupitia video hii Professor Jay anaweka bayana hali mbalimbali za kimaisha na matokeo yake.Kuna kupanda na kuna kushuka.Usimdharau mwenzako asiyenazo hii leo kwa sababu hujui kesho utakuwa wapi na katika hali gani.Yote anapanga Muumba.Pia Pro.Jay anakemea sio tu hali hiyo bali pia hata kitu ambacho kwa mapana na marefu kiliitia doa nchi yetu.Ni kitendo cha baadhi ya binadamu kuwageuza wengine kuwa “dili”.Kitendo cha wapuuzi fulani kuwaua albino kwa imani potofu kabisa za kishirikina na kupata utajiri.Itizame video hii na kisha usisite kutoa tathimini yako.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...