Usiku wa kuamkia leo Moto ambao haukufahamika chanzo chake uliteketeza soko dogo lililopo maeneo ya Forest ya zamani karibu na Chuo kikuu cha Mzumbe na Chuo Kikuu huria matawi ya Jijini Mbeya na kusababisha mabada kadhaa kuteketea kwa moto ambao uliwahiwa na kikosi cha zima moto cha mkoa wa Mbeya.
Mkuu wa wilaya ya Mbeya Mjini,Bw. Evans Balama alifika katika eneo hilo usiku huo na kusaidiana na wananchi waliokuwepo karibu na eneo la tukio na kuuzima Moto huo kabla ya kikosi cha zima moto kufika eneo la tukio.Kumekuwa na maswali mengi sana hivi sasa Jijini Mbeya ya kujiuliza,kunani katika masoko ya Mbeya mpaka kila siku yawe yanawaka moto na kwanini tahadhari hazichukuliwi mapema??
Kamera man wa Globu ya Jamii ambaye alifika eneo la tukio mapema leo asubuhi na kukuta moto umefanikiwa kuzimwa katika vibanda hivyo vilivyokuwepo sokoni hapo na haya ndio baadhi ya masalia ya mabanda hayo huku moshi ukiendelea kufuka.
Mashuhuda waliokuwepo maeneo ya jirani na soko hilo walisema Moto huo ulianza majira ya saa 9:00 kamili usiku na muda si mrefu taarifa ziliwafikia kikosi cha Zimamoto na wao walifika eneo la tukio dakika 10 baadae na kufanikiwa kuuzima moto huo bila hata ya maigizo yao ya kila siku ya kufika eneo la tukio bila ya kuwa na maji au kuharibika kwa gari wakati wakiwa kwenye tukio.Picha na Latest News TZ

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hapa sio bure kKna mchoma moto (arsonist) kazini. Jee anafanya hivyo kwa maslahi ya nani, yake au katumwa?

    Wengine hupenda tu kuona watu wanavyohangaika pale vibanda vinavyoungua. Dunia ina mambo.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...