Transforma iliyopo ndani ya uzio wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Imeripuka mchana wa leo na kufanya wafanyakazi wa Shirika hilo kukimbia huku wengine wakijaribu kufanya utaratibu wa kuuzima moto uliokuwa ukiwaka kwenye Transfoma hilo.Hii ni mara ya pili kulipuka kwa Transfoma hilo baada ya juzi jumanne kulipuka na kuwahiwa kuzimwa.


Inaelezwa kuwa transfoma hiyo iliyoripuka leo ni mpya baada ya kubadilishwa ile ya awali iliyowaka juzi. wachina wa Star Times ndiyo waliotaharuki zaidi kwani ofisi zao almanusura ziungue kutokana na ukaribu wa na Transfoma hilo.

Baadhi ya ofisi za TBC, ambazo ziko jirani na transforma hilo zimeungua moto.Kikosi cha Zima Moto Kama kawaida yake kilifika eneo la tukio kwa kuchelewa na kukuta baadhi ya sehemu zishaungua kwa moto huo.

Kwa Sasa moto huo ushazimwa na taratibu zingine zinaendelea ili kujua nini chanzo cha kuungua kwa Transfoma hilo.

 Moto ukiendelea kuwaka kwa kasi.
Moshi mzito ulitanda angani wakati Transfoma hilo linawaka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. ukitaka kuzima moto kwa fire extinguisher, AIM AT THE BASE, sio juu kama hao jamaa!

    ReplyDelete
  2. Tanzania zimamoto is a joke! Lini waliwahi kuzima moto?

    ReplyDelete
  3. Transforma litawakaje wakati hakuna Umeme? ahem.

    ReplyDelete
  4. SASA KAMA MNANUNUA CHINA HIZO TRNSFORMER MNATEGEMEA NINI? MARA MKO SASA BRAZIL UFISADI UKO PALE PALE NA HAO IWE KAMA DOWANS SAWA KABISA KWANINI MNAWAOGOPA WAZUNGU? KWANINI TWA WAONA KAMA KITUO CHA POLISI KWA SABABU HAMUWEZI KUFISADI KAMA WAO WAKICHUKUA JUKUMU HILO

    ReplyDelete
  5. Duu! Hii ni hatari. Maana hao wanaozima huo moto bahati yao, wangenaswa na wao. Moto wa umeme wanazima kwa maji tena wakiwa karibu kabisa na transfoma bovu

    ReplyDelete
  6. ANKO MICHU TUELEZE VIZURI HILO TRANSFORMER NI JIPYA AU SECOND HAND KAMA KAWAIDA YETU? BASI KAMA NI JIPYA LAZIMA NI MADE IN CHINA

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...