Rais Jakaya Kikwete akipokea maelezo kutoka kwa Meneja Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Salum Mwalim kuhusu mchnago wa kampuni hiyo katika kuunga mkono mpango wa serikali wa kushawishi uwekezaji katika ukanda wa ziwa Tanganyika wakati rais Kikwete alipotembeela banda la Vodacom wakati wa maonesho yaliyofanyika pembezoni mwa kongamano la uwekezaji ukanda mpya wa uwekezaji ziwa Tangayika uliofanyika jana Mjini Mpanda na kufunguliwa na Rais Kikwete.Katikati ni Meneja wa M-PESA mikoa ya Ruklwa na Katavi
Rais Jakaya Kikwete akifungua kongamano la uwekezaji katika eneo jipya la uwekezaji kanda ya ziwa Tangayika jana Mjini mpanda mkoa mpya wa Katavi. Zaidi ya wajumbe mia tatu kutoka sekta mbalimbali ndani na nje ya nchi walihudhuria kongamano hilo ambapo fursa za uwekezaji katika mikoa ya Kigoma, Rukwa na Katavi ziliainishwa na kujadiliwa kwa kina. Vodacom ilishiriki kuwezesha kongamano hilo.
Sehemu ya mabalozi na wawekezaji wakifuatilia hotuba ya Rais Jakaya Kikwete (hayupo pichani) ya ufunguzi wa kongamano la uwekezaji katika ukanda wa ziwa Tanganyika uliofanyika jana mjini Mpanda. Zaidi ya wajumbe mia attu kutoka sekta mbalimbali ndani na nje ya nchi walihudhuria kongamano hilo ambapo fursa za uwekezaji katika mikoa ya Kigoma, Rukwa na Katavi ziliainishwa na kujadiliwa kwa kina. Vodacom ilishiriki kuwezesha kongamano hilo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...