Na Mwandishi Wetu
 
CHAMA cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) leo kimewakutanisha wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini kujadili ukatili wa kijinsia kwa jamii.
 
Hatua hii ni moja ya programu ya Kihistoria ya Siku 16 za wanaharakati kupinga ukatili wa kijinsia kwa jamii ambayo ilianzishwa tangu mwaka 1991 na Kituo cha Kimataifa cha Wanawake katika Uongozi (Centre for Women’s Global Leadership).
 
Akizungumza katika semina hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Ananilea Nkya (pichani) amesema lengo la semina kwa wahariri hao ni kuhakikisha wanafahamu mchango wa wanaume katika kupambana na ukatili wa kijinsia nchini Tanzania.
 
Akifafanua zaidi Mkurugenzi huyo alisema lengo lingine ni kuhakikisha wahariri wanakuwa mstari wa mbele kuanzia Novemba 23 hadi Desemba 10 kuwaamsha kiutendaji pande husika kuchukua hatua juu ya vitendo hivyo vya kikatili.
 
Aidha mada anuai zimetolewa kwa washiriki ili kujenga uelewa juu ya namna ya kutumia nafasi zao kwa vyombo vya habari na kuleta mabadiliko katika suala zima la ukatili wa kijinsia ambalo limekuwa likiwaathiri zaidi wanawake na wanafunzi hasa wa kike.
 
Kauli mbiu ya maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia ni “Miaka 50 ya Uhuru: Pinga Ukatili Kuimarisha Tanzania Huru”.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. huyu mwanamke kihere here sana i hate her.

    ReplyDelete
  2. Hata mie simpendi kweli, anauma na kupuliza hana jipya zaidi ya jazba tu na chuki za kijinga.

    ReplyDelete
  3. Ukweli unauma!
    Tena Madam endelea na Mapambano.
    Wa mama wengi wanakufa kwa kufanyiwa ukatili Mkubwa vijana kwa wazee wanaambukizwa ukimwi, hawana pa kujitetea na hawajui wafanye nini,wanachanganywa na Mabinti zao,watoto,H'made na wadogo zao. Jamii imechafuka!!!
    Endeleza Mapambano.

    ReplyDelete
  4. Huyu ni chadema damu hivi kweli ana tetea au unafiki? mbona swala la mkuu wa wilaya alivyodhalilishwa hakusema kitu?

    ReplyDelete
  5. nyie wote mnaomchukia huyu mama mtakuwa mafisadi pia hamna jipya. Maana hampendi Ukweli

    ReplyDelete
  6. yeye wenyewe ni dictator wenzake hawapendi kakatilia kwenye cheo huku anajifanya ni champion wa democracy

    ReplyDelete
  7. Huyu ni kibaraka wa chadema, hamjui hilo, Mbona ya kule Tabora hakusema? Yule alinyanyaswa sio mwanamke? Mzandiki mkubwa!

    ReplyDelete
  8. Mimi ni mwana chama wa TAWA na weza kusema kuwa huyu mama ni mnafiki, mdini, na chadema, hana kutetea haki wala nini, sisi wenyewe kwa huyo mama tunaipata laivu, ni mroho wa madaraka hivyo hapo alipo anategemea labda chadema ishinde achukue nafisi ya Mh Sofia Simba hili tunamuombea kila siku lisiwe na inshallah Mwenye enz Mungu atalisikia.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...