Mkazi wa Kijiji cha Mkanyageni Mkoani Tanga ambaye jina lake halikuweza kupatikana,akichafua mazingira kwa kutupa takataka katika mto uliopo katika eneo hilo kama alivyokuta na kamera man wa Globu ya Jamii ambapo alipobaini kuwa anapigwa picha alianza kuficha sura yake huku akiendelea na shughuli yake ya kutupa taka hizo bila uoga wowote.
Hapa ndio hakutaka kabisa kuonekana.


sababu ya elimu duni
ReplyDeleteinafahamika kabisa ni kosa kutupa taka ovyo!...? Je huyo cameraman alichukua uamuzi gan zaidi dhidi ya mtu huyo??? Au ndo aliishia kupiga picha tu???...
ReplyDeleteWewe Cameraman ulimchukulia hatua gani huyo mpuuzii
ReplyDeleteTanzania chafu inawezekana
ReplyDeleteKithibiti kipo hicho, na nyie watu wa Tanga mwamjua huyo; mwataka mpiga picha akamkamate avunjiwe kamera yake?!!?
ReplyDeleteKamwulizeni Jery Muro!!
Usiwaone hivyo hao, kwanza hali yake tu inafanana na shari. Ona, anajua kabisa anapigwa picha lakini hatishiki bali aficha uso tu, nyie mwadhani mtu mwema huyo. Mchunguzeni upamba aliouficha kiunoni kwanza, mwataka mpiga picha apoteze damu yake?
Watu wengine bwana, ungekuwa wewe ungemsogelea? Mnajua kulaumu tu na kusuta watu. Mnapiga kelele ndani ya chumba, mbona hujaandika jina lako hapo kama kweli ungefanya lolote?
ReplyDeleteTanga kulee, kunani kulee?
Moneni yule anayemwangalia toka kwenye nyumba ile, yule ndiye anafaa kuchukuwa hatua mara moja kwenda kumkamata. Mpiga picha anathabarisha tu, kwa wasiotambua utunzaji wa mazingira.
ReplyDeleteHuyu ni bingwa wa wachafuzi wa mazingira kule kwao.
picha hii imenikumbusha mpiga picha aliyeenda sudan kuandika madhara ya njaa na kumkuta mtoto aliyelemewa na njaa huku pembeni kuna tai(ndege) akimsubiri afe ili amle,yule mpiga picha alichofanya alichukua picha nzuri ya kuuonyesha ulimwengu hali ya njaa ilivyokuwa.Mwanzoni alisifiwa sana kwa kufikisha ujumbe mzuri kwa watu,lakini baadaye wachambuzi wa mambo walipoanza kuhoji kwanini hakumwokoa yule mtoto asiliwe na tai badala ya kukazania kuchukua picha tu,alikosa jibu,akasononeka ,mwishowe nilisikia aliamua kujiua kwa kugundua kosa alilolifanya.Sasa swali mpiga picha ulichukua hatua gani dhidi ya mtu huyu adui wa mazingira na maisha ya watu ?au ulifurahia kumpiga picha tu!!!!!
ReplyDeletewee mpiga picha kama hukumchukulia hatua yoyote tafadhali nyofoa lipicha lako mara moko!
ReplyDeleteMpiga picha kafanya kazi yake mengine sio ya kwake na hana nyenzo za kufanya zaidi ya hapo. Wahusika waanzie hapo!!!
ReplyDeleteNyie vipi kazi ya kamera man si kufikisha ujumbe? sa mnataka afanye nini zaidi?
ReplyDeleteWafuasi wa CHADEMA hao na ukimwambia lolote kama una gari litavunjwa na camera yako halafu siku ya pili maandamano kuvunjia watu maduka yao.Upsss nimesahau kama wamekuwa mke wa pili na maandamano yamekwisha.
ReplyDeletempiga picha kafanyakazi kubwa na ya muhimu. Next ni dola.Tuko pale pale nchii hii sheria hazisimamiwi. Ela imechukua nafasi ya sheria
ReplyDeletePAMBAFU KABISA!!!SIJUI NISEME HUYU KAKA AKAMATWE NA KUPIGWA MIJELEDI KADHAA AU NISEME ATIWE DARASANI NA KUFUNDISHWA SOMO LA MAZINGIRA NA HIFADHI ZAKE?
ReplyDeleteNAONA BORA YOTE MAWILI YANAMHUSU HUYU KAKA
sasa mnataka atupe wapi nawakati system mbofu, na hisitoshe hizo takataka si mmempawenyewe, mlijua anaenda kuzitupa wapi?huyo jamaa anafanya kazi naye ,kwani taka taka si nikazi ya jiji au kila mtu anatakiwa kuipeleka taka taka dampo mwenyewe?
ReplyDeleteJamani msameheni huyu jamaa, Kwa jinsi alivyo na mavazi yake sidhani kama ana akili timamu.
ReplyDeletehapa ni daraja la pale Hale, jirani na kituo cha uzalishaji umeme cha pangani falls
ReplyDeleteNi keli ni uchafuzi wa mazingira na inafaa kuchukuliwa hatua. Na hata kama si mtoni uchafu ni uchafu tu! Ila,nimezaliwa Mkanyageni, nimekulia Mkanyageni lakini ninawasiwasi na huo mto unaopita katikati ya nyumba au kijiji sijapata kuuona. Naomba mpiga picha ataje jina la huo mto. Naujua mto kivumiro na sijapita siku nyingi sina ila sidhani kama kumeshajengwa kwa kiasi hiki. Au siyo Mkanyageni ya Wilaya ya Muheza kata ya Ngomeni tarafa ya Ngomeni?
ReplyDeleteASANTE SANA MPIGA PICHA KWA KAZI NZURI SANA. UMEMALIZA JUKUMU LAKO. MGAWANYO WA MAJUKUMU (DIVISION OF LABOUR"
ReplyDelete