Mkongwe wa muziki wa injili Afrika Mzee Cosmas Chidumule pamoja na mwalimu maarufu wa Muziki wa injili afrika mashariki bwana John Shabani,Wamegusa mioyo ya maelfu ya waumini walioshiriki ibada katika kanisa la mlima wa moto (Mountain of fire) la Mikocheni B Assemblies of God linaongozwa na Dr, Rv. Getrude Rwakatare. Kibao cha Kwa Yesu kuna raha chake john Shabani alichomshirikisha Chidumule ndicho kilicho tifua maelfu ya waumini hao. Wimbo huo umo ndani ya album mpya yakwake John shabani alioshirikisha waimbaji nyota wa nyimbo za injili Tanzania, Congo na Uganada. Album hiyo inatarajia kukamilika mwishoni mwa mwaka huu kwa mfumo Audio na video na inasimamiwa na kusambazwa na Kampuni ya Msama Promotions

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. michuzi turushie hapo walau kawimbo kamoja tuburudike ndani ya Yesu!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...