NGORONGORO YAANZA KWA SARE

Tanzania (Ngorongoro Heroes) imeanza kwa sare michuano ya Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Kusini mwa Afrika (COSAFA) kwa vijana chini ya miaka 20 inayofanyika Gaborone, Botswana.

Jana (Desemba 2 mwaka huu) katika mchezo dhidi ya mabingwa watetezi Zambia uliofanyika Uwanja wa Chuo Kikuu cha Gaborone, timu hizo zilitoka sare ya kufungana mabao 3-3.

Mabao ya Ngorongoro Heroes yalifungwa dakika ya 2 na 13 kupitia kwa Simon Msuva. Bao la tatu lilifungwa na Hassan Dilunga dakika ya 40. Evans Kangwa aliifungia Zambia mabao mawili wakati la kusawazisha lilifungwa na Alex Sichone.

Ngorongoro iliwakilishwa na; Jackson Wandwi, Hassan kKessy, Issa Rashid, Samuel Mkomola, Frank Raymond, Atupele Jackson, Simon Msuva, Amani Kyata, Edward Shija, Frank Sekula na Hassan Dilunga.

Tanzania itacheza mechi ya pili Desemba 4 mwaka huu na Afrika Kusini wakati ya mwisho katika hatua hiyo ya makundi itakuwa Desemba 6 mwaka huu dhidi ya Mauritius.

Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. hii tff haina mtandao? kama upo basi mnisamehe msiniangukie kama mawe yaliyounga njia huko eeee wapi vile?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...