Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Robin Goetzsche (kushoto), akiwawashia mishumaa wafanyakazi wa kampuni hiyo, wakati wa maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani yaliyofanyika Makao Makuu ya TBL,jijini Dar es Salaam juzi.
Mkurugenzi wa Fedha wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Kevin O'Flaherty (kulia) akiwasaidia wafanyakazi wa kampuni hiyo kuwawashia mishumaa wakati wa maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani yaliyofanyika Makao Makuu ya TBL, jijini Dar es Salaam juzi.
Wafanyakazi wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), wakiwasha mishumaa wakati wa maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani,katika Makao Makuu ya kampuni hiyo, jijini Dar es Salaam juzi.
Meneja wa Kiwanda wa TBL, Bw. Rweyemamu (kulia) akimpatia Ofisa Usalama mahali pa Kazi TBL,Ismail Kalembo zawadi ya simu aina ya BlackBerry, baada ya kuwa mmoja wa wafanyakazi wa waliopima kwa hiari virusi vya Ukimwi.
Meneja Mauzo wa TBL, John Mgega (kushoto) akimpatia zawadi mfanyakazi Khadija Maulid ambaye ni mmoja wa wafanyakazi walioamua kwa hiari yao kupima virusi vya ukimwi.
Mama mhamasishaji vita dhidi ya UKIMWI,akimpatia zawadi ya bia mmoja wa wafanyakazi wa TBL.
Wanakamati ya maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani, kwa upande wa TBL,wafanyakazi wa TBL,WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA BAADHI YA WAATHIRIKA WA UKIMWI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Bia si ndiyo kichocheo chenyewe haswaaaa.

    Mtu akishaujaza kichwani hapo sketi itakayopita mbele basi haitakuwa na salama.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...