mwili wa marehemu Twahir Hussein Omari, maarufu kwa wengi kama "Mboga Zote" hautaweza kuwasili nchini leo kama ilivyokuwa imepangwa hapo awali,kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wa Jumuiya ya Watanzania nchini Italy ambao ndio walikuwa na jukumu la kuusafirisha mwili huo kuja hapa nchini kwa Maziko.Globu ya Jamii inaendelea kuwasiliana na Wadau wa Jumuiya ya Watanzania nchini Italy ili kufahamu yale yaliyoyotokea na ni lini Mwili utasafirishwa na kuwasili nchini kwa ajili ya taratibu za Maziko.
hivyo tuendelee kuvuta subira mpaka hapo taratibu zote zitakapokamirika.
kama mambo yamekuwa magumu huko nje jamani rudini nyumbani.
ReplyDeletePoleni sana na huu msuko suko Watanzania wa Italia.
ReplyDeletekwa taarifa zaidi mwenyekiti wa watanzania waishio Modena Mzee Paskal Nyalusi,yupo Tanzania kwa taarifa zaidi piga 0767 242864
ReplyDeleteananymous wed 18 jan,hivi wewe unaakili timamu unaposema watu warudi nyumbani maisha huko magumu kwani hapa nyumbani ndio rahisi,kazeni buti vita mbele hapa kama una ndugu mbunge au yupo serikalini njoo,lakini hizo facilities mnazo pata huko hapa bado ni ndoto kama haupo kwenye system si mnaona mara kibao mtu achangiwe iliakatibiwe au viongozi wakiumwa wanatumwa huko ulaya huo mfano tu 1 ipo mingi sasa si bora ukae karibu na uduma muhimu za binaadamu huku maji tabu,umeme nk waache bwana mabaharia wachakalike
ReplyDelete