·        Kampuni pekee ya kizalendo iliyoweza  kuwasaidia watanzania waliotapeliwa na makampuni ya Kijapani lakini kwa msaada wetu wamepata haki zao.

·        Kwa waliotapeliwa hela zao na hawakupata gari zao kuanzia mwaka 2008 mnakaribishwa mkiwa na vielelezo vyote vilivyotumika wakati wa mauziano.

·        Ofisi zetu kwa Dar  Es Salaam tunapatikana mikocheni, Kwa Japan tunapatikana Osaka.
Kwa mawasiliano zaidi wasiliana nasi kwa simu zifuatazo;
      Tanzania:  +255 713 335 474 / +255 757 714 410
       Japan:  +818037627895.

Karibuni sana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 33 mpaka sasa

  1. Kampuni inaitwa nini? Website? Kwa nini email addresses zenu zimekaakaa ki-a.k.a.? Mikocheni sehemu gani? Si rahisi mkaaminiwa namna hii.

    ReplyDelete
  2. Ukishaibiwa na mwizi mmoja, na wa pili anatafuta kukuibia kidogo ulichobaki nacho.

    ReplyDelete
  3. Hiyo namba ya simu ya Japan ni mobile phone. Hawa nao watakuwa ndo walewale.

    ReplyDelete
  4. Tutegemee nini kumpa chui atuvushie mbuzi wetu mtoni? Tuwe macho watanzania, wajanja watatumalizia hawa.

    ReplyDelete
  5. Msaada pekee ni kutumia kampuni za wanasheria waliopo huko huko japan.
    Hawa madalali wanaotafuta pesa ya Ugali hawana msaada wowote zaidi ya kuwaongezea watu hasara ya pesa zao.

    ReplyDelete
  6. Duh! wabongo kwa kutengeneza dili hawajambo.
    Hapa tusubili tu kusikia watu wameachwa solemba.
    Bongo tambarare!!

    ReplyDelete
  7. Mambo vp mzee Mcheri? Nitafutie prado ya 97.
    Kama upo Bongo naomba unipigie.
    Wambura wa Tabata.

    ReplyDelete
  8. Big Up Mcheri. Naona Lucus mnajitahidi sana kuuza magari. Ila haya mambo ya sheria umeanza lini kaka?

    ReplyDelete
  9. Michuzi inabidi uwe makini kuzihakiki taarifa unazopewa kabla ya kutuletea.. maana hizi namba za Tanzania zinazoanzia 0713 na 0757 ni mobile phone, sasa usalama upo hapa kweli??
    Tusiwaongezee matatizo waliopatwa na matatizo.

    ReplyDelete
  10. Hii dili imekaa kimtego mtego. Tujiandae kusikia watu wanalizwa mara ya pili. Wabongo bwana.. we acha tu!

    ReplyDelete
  11. Safi sana Papaa Mcheri mokili nakuaminia baba kwa ubunifu wa kuzisaka ngawila. Piga kazi kijana tuendelee kula bata kwa kwenda mbelee..

    ReplyDelete
  12. Hongera sana. Nawaaminia sana hawa lucus japan kwa marketing strategies zao. Inabidi mzee jumanne utufundishe na sisi wabongo wenzako haya ma-techniques ya huko Osaka ili tunyanyue maendeleo ya Bongo.

    ReplyDelete
  13. wabongo wa huko osaka na nagoya hawaachi tu longolongo zao. Namba za simu walizoandika za japan na bongo zote ni mobile phones. Jungu linalopikwa hapa ngoja tutege masikio.

    ReplyDelete
  14. Michuzi, hutakiwi kuweka tangazo kama hili. Linaonekana ni sanaa tupu....


    Mdau DC.

    ReplyDelete
  15. Jumanne WaryobaJanuary 05, 2012

    Michuzi ongeza basi taarifa za hao jamaa. Maana wengi tumeshaumizwa kwa kununua magari kwenye mtandao wa Tradecarview.

    ReplyDelete
  16. Mcheri MokiliJanuary 05, 2012

    Watanzania wenzangu tuchangamkie hii dili kuokoa pesa zetu. Tuwasiliane na hawa jamaa kwenye hizo namba zao za simu.

    ReplyDelete
  17. Haujaacha tu yale mambo yako papaa mcheri japanese. Grow up man.

    ReplyDelete
  18. Lengo langu ni kuwasaidia watanzania wenzangu waliopoteza pesa zao pale kwenye mtandao wa tradecarview.
    Hivyo msione kama nataka kuwatapeli pesa zenu.

    ReplyDelete
  19. Ubalozi wa Japan hapa Tanzania na ule wa Tanzania kule Japan wameshindwa kutatua haya matatizo nyinyi ndo mtayaweza kwa kutumia hizo ofisi zenu za kwenye mobile phone? Acheni utoto jamani kwenye mambo serious kama haya. Michuzi vp kaka unashusha hadhi ya blog yako kwa kupost upuuzi kama huu.

    ReplyDelete
  20. Hebu toeni pumba zenu za kitapeli

    ReplyDelete
  21. Grow up mokili

    ReplyDelete
  22. Hongera sana vijana wa nagoya kwa ubunifu wa sanaa za kipigaji.

    ReplyDelete
  23. recession inayoendelea huko japan, wabongo waliopo huko watatoana macho kwa michoro kama hii ya maji taka. ajira hakuna biashara zimedoda. mrudi tu huku nyumbani muanze upya.

    ReplyDelete
  24. Hawa wahuni wenye hii post wananikumbusha.. wimbo wa profesa J.. "Aliyeuza cheni kapewa fedha bandia na aliyununua kapewa cheni feki. Hapo ni ngoma draw ndani ya bongo darisalamu"

    ReplyDelete
  25. Wazee wa Azam Takeaway pale mtaa wa jumhuri wameadvance shughuli zao mpaka kwenye michuzi blogu!! Si mchezo, kwa mtego huu watawapiga vipofu wengi.

    ReplyDelete
  26. Segerea inawaita hawa wenye hizi mobile numbers. Siku hizi simu zote ziko registered sijui watakimbilia wapi hawa wasanii.

    ReplyDelete
  27. ............... Papaa Mcheri, tupe gharama za huduma hii !
    ...... Ankal weka angalizo kuwa "Blog yako haitahusika kwa njia yeyote na sanaa hii, Buyer be......"

    ReplyDelete
  28. Hawa ni LUCUS T (LTD)wako opposite shoppers, nawapongeza kwa ubunifu wenu...ila mmeshafanya research ya kutosha ya mnachokiadvertise?

    Nawajua mko vizuri kweny biashara ya magari kwa kuwa nimeshafanya nanyi biashara...ila kwa hili sina hakika.

    ReplyDelete
  29. WAAGIZA MAGARI WAKOME SASA:

    Unakuta mtu ana pesa ya kuunganisha, labda amewazima wenzie ktk dili, amedunduliza ameuza bidhaa za jumla,msimu wa mauzo wa mazao, amekopa Saccos, ana pesa ya ngama labda mafao baada ya kumaliza mkataba wa kazi,analipwa Mil. 10 yake,,,huyo anaingia ktk mtandao anatuma hela yote kuagiza gari!

    Badala ya pesa hiyo ya bahati Mil.10 kufungua hata genge la bamia na dagaaa linalozungusha vizuri kwa Mil. 2.5 hivi na zingine Mil.7.5 akaweka akiba benki!

    WATANZANIA KWA KUPENDA KIJIKO, MUONEKANO, UMAARUFU NA SIFA SISI HATUJAMBO!

    ReplyDelete
  30. Lakini biashara ya genge , ndiyo biashara salama kwa mstaafu, nayo ataliwa tu, tofauti atakuwa anatafunwa mtaji wake taratibu bila yeye kujijua. Taabu yetu, watanzania ni kusubiri hadi ustaafu ndiyo ufanye, kama mtu anaweza biashara ya genge au yoyote kwani usianze ukiwa kazini?? Matokeo ya kutoanza mapema, ndio mtu anapamia mambo oh ngoja niagize gari Japan, huko nako anakuta matapeli na kuliwa.

    Tuwatumie watanzania wenzetu kutushauri katika mambo mengi na usione hasara kumlipa mtu kidogo ukaookoa hasara kubwa mbeleni.

    ReplyDelete
  31. Janja wewe iko!
    Je unaujua mwimbo wa watoto..
    Buibui kasema kwa nzi karibu ndani
    Nimepamba nyumba yangu.....

    ReplyDelete
  32. Ndio ndio wenye hamu ya kulizwa acha waendelee na mtoto akililia wembe mpe ili ukimkata ndipo atatia akili.

    ReplyDelete
  33. Hawa wanaotangaza kusaidia waliotapeliwa magari Japan halafu anwani waliyotoa ni simu za kiganjani, ndiyo wale wale walioenda kwenye msiba wakaiba majamvi. Jamani muangakie msije mkalia mara ya pili.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...