Namshukuru sana mwenyenzi mungu (S.W.T) kwa kutufikisha siku ya leo tarehe 14/2/2012 (valentines day),ambapo leo tumetimiza miaka miwili ya ndoa na kujaaliwa watoto wawili,Lemmysa alizalliwa tarehe 25/9/2010 na bahati pia alizaliwa tarehe 5/12/2011.Hatuna cha kumlipa Mungu,bali ni kumshukuru na kumuomba atupe maisha marefu ya ndoa na niendelee kumpenda Mke wangu Zeenat milele na wanangu awape malezi mema na maisha marefu. Asanteni,Nawatakia Happy Valentines Day njema.
Bahati sigh.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. God bless this family, Happy Valentines to you. bll

    ReplyDelete
  2. DU HII KALI KILA MWAKA MTOTO, ??? HONGERA

    ReplyDelete
  3. Nikiangalia hesabu ya hizo birthdays za watotot wako mmmmh! Inabidi muumwone mama Ushauri haraka.

    ReplyDelete
  4. Na mkeo akupende pia....Great familly

    ReplyDelete
  5. Duuh jamaa kiboko, kwa muda wa mwaka 1 na miezi miwili na nusu mmepata watoto wawili!! Hii speed ni kali mno.

    ReplyDelete
  6. Mhn!.......COMMENT RESERVED!.

    ReplyDelete
  7. hongerani kwa kutimiza miaka 2 ya ndoa, mmependeza kwa kweli

    ReplyDelete
  8. Inapendeza sana tunawashukuru kwa kutukumbuka...sisi ndoa zetu ni vita kila kulicha. ndugu wa mume wamefanya ndoa yetu kuwa jehanamu.

    ReplyDelete
  9. KAKA umependeza sana na familia yako, ila kama wewe ni Muislam, valentine day ni haramu kusherehekea.

    ReplyDelete
  10. kaka, nitakuwa sijaangalia vizuri au macho yangu yananiongopea? naona kama miaka 2 ya ndoa watoto 2! mbona kama mmekwenda haraka? mtoto anatakiwa anyonye at least miaka 2 kamili halafu jitihada za kutafuta mdogo wake ndio zinaanza, hongera!

    ReplyDelete
  11. miaka miwili ya ndoa ,watoto wawili!!!!!???? kali lakini hongera!

    ReplyDelete
  12. Insha'Allah Mwenyezi Mungu akukuzieni watoto wenu na wawe kizazi bora,,na mja'aliwe kuongezewa tena wengine wawili waje kucheza na hao wenzao
    Mimi nimewapendaje!jamani Nice couple!mwanzo juzi niliwaona katika 8020fashion nikamuuliza sister wangu aangalie mlivyotoka vizuri katika picha,,
    Duah yenu Mola akupokeleeni,,na sisi pia!
    Ahlam,,,UK

    ReplyDelete
  13. inamaana huyo wa kwanza ulimzaa kwa miezi saba au uliibeba kabla ya ndoa.
    Kama wewe ni muislam, basi valentain sio desturi ya waislam ni mila za makadiyani.

    ReplyDelete
  14. Inshallah AMIIIIIN,

    Mwenyezi Mungu atawajaalia!

    Cha msingi katika Uzazi ni afya bora ya watoto na sio hatua au muda kati ya mtoto anayefuata aliyemtangulia kuzaliwa.

    Katika picha hapo Wadau mnaona wenyewe watoto wote wawili wapo bukheri wa afya na hakuna dalili zozote za hitilafu ya kiafya kwa watoto.

    SASA KWA TAARIFA YENU HUU NDIO UZAZI WENYE TIJA!

    ReplyDelete
  15. Lovely family! like that endeleeni hivyo hivyo msiache gap mpaka mmalize mliopanga kazi ibaki kulea sio mtu anakaa miaka kibao ndo anawaza tena jinsi y akufunga nepi that one is marvelous.

    Mungu awajalie maisha yenye furaha na amani.

    ReplyDelete
  16. jamani hongereni sana,pia kama wazazi wa kisasa au wasomi,tumieni uzazi wa majira msiwe kama watu ambao hawajachungulia shule kabisa.

    ReplyDelete
  17. mmependeza sana, Bahati naona kama umevaa chain ya dhahabu, kama ni kweli mwannaume sio vizuri kuvaa. Vaa silva na mama mnunulie dhahabu za kutosha.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...