AZANIA BANK LIMITED

Uongozi wa Benki ya Azania, (Azania Bank Ltd) unapenda kuwataarifu wateja wake na umma kwa ujumla kwamba kuna ujumbe wa simu (sms) unaotumwa kwao kutoka simu namba 0023222291029 ya kwamba wameshinda zawadi na wapige namba hiyo kufuatilia hiyo zawadi. 



Benki ya Azania inawajulisha watu wote kuwa haihusiki na ujumbe huo na yeyote atakayeupata ujumbe huo asiujibu na aufute mara moja wakati tukiwasiliana na mamlaka husika kwa ufumbuzi zaidi. 


Tunaomba radhi kwa usumbufu unaojitokeza.

IMETOLEWA NA UONGOZI WA AZANIA BANK LTD.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Usanii mwingine Jamani, kama huu wa simu na meseji watampata nani?

    Si bora waende shamba wakalime tu?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...