Mkurugenzi wa U-turn blog Mange Kimambi na Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wakifurahia pamoja na watoto yatima walipofika katika kituo cha kulelea watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu cha Kurasini jijini Dar es Salaam,msaada wa vyakula na vitu mbalimbali uliokuwa na thamani ya shilingi Milioni 10 ulitolewa na U-turn blog kwa ushirikiano wapamoja na wasomaji wakuu wa Blog hiyo.
Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba akiwa amebeba mmoja wa watoto yatima wanaolelewa katika kituo cha kulea watoto yatima cha Kurasini jijini Dar es salaam.Wakati wa blog ya U-turn kwa kushirikiana na wasomaji wake wakuu walipokwenda kutoa msaada wa vitu mbalimbali vikiwemo vyakula na nguo vyenye jumla ya thamani ya shilingi Milioni 10.

Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba akiwa na watoto yatima wanaolelewa katika kituo cha kulea watoto yatima cha Kurasini jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi wa U-turn blog Mange Kimambi na Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wakifurahia pamoja na watoto yatima walipofika katika kituo cha kulelea watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu cha Kurasini jijini Dar es Salaam,msaada wa vyakula na vitu mbalimbali uliokuwa na thamani ya shilingi Milioni 10 ulitolewa na U-turn blog kwa ushirikiano wapamoja na wasomaji wakuu wa Blog hiyo.
Mkurugenzi wa U-turn blog,Mange Kimambi akizungumza na Watoto hao

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 16 mpaka sasa

  1. Huyo Dada ni Mdogo wake Mwamvita mbona wanafanana sana?

    ReplyDelete
  2. Mange na Mwamvita,

    Ahsanteni kwa Msaada na Ubinaadamu wenu!

    Mwenyezi Mungu Mkuu atawazidishia!

    ReplyDelete
  3. Mmmmmh!

    "Mkurugenzi Mkuu" wa Blog?!?
    Hivi mnaelewa nyinyi maana na hadhi ya hilo neno au munajiandikia tu?

    Hebu nendeni kule BRELA wawafafanulie maana ya "Mkurugenzi"

    Mweeh!

    ReplyDelete
  4. Nataka nipeleke posa kwa Mzee Makamba. Je Mwamvita yupo "single"?

    ReplyDelete
  5. Mwanvita huyo mtoto uliyempa miwani amependeza sana..Tuwapende watoto siyo siri.Baada ya miaka 30-50 hao ndiyo watakuwa wanaongoza nchi yetu tuipendayo.Vodacom mkipata faida si vibaya mkawapeleka pale xxxx barabara ya Nyerere.kuna michezo yao mingi sana,watafurahi sana ila 'bei'!!?

    David V

    ReplyDelete
  6. hONGERA sana wadau wa u-turn na Mange kwa kufanikisha hiyo siku. mmeonyesha moyo na upendo mkubwa sana kwa hao malaika. mbarikiwe wote na msiishie hapo. na hii iwe changamoto kwa wengine wenye nia ya kufanya kama wana u-turn. Ujumbe; EDUCATION IS SEXY

    ReplyDelete
  7. Mbarikiwe sana kwa kuwapa yatima upendo

    ReplyDelete
  8. Mdau wa 3 hapo juu Mlevi,

    Ukurugenzi wa Kampuni sio kuwa na koti kubwa au muonekano wa kuwa na kitambi, kinachotakiwa ni uenezi wako hata kama umevaa Gunia!

    Wapo Mabosi wangapi ambao hata Shs. 100/= yao ni vigumu kuitoa kwa Wahitaji katika Jamii yetu?

    ReplyDelete
  9. Hawa Madada Mange na Mwamvita kazi wameifanya!

    Sio mchezo kukusanya kiasi hicho cha fedha Mil. 10 na ukazifikisha kunako husika, yataka jitihada na moyo safi!

    Kwa wengine kwa mtaji huo wangezitia kibindoni na kuwahi kwenye Yadi kununua gari!

    Kweli wameteuliwa!

    ReplyDelete
  10. Hivi hapa nani anamsaidia nani???? TAFAKARI

    ReplyDelete
  11. Joka la MdimuFebruary 14, 2012

    wewe david v Acha mambo yako Mwamvita napeleka posa mimi
    tena ngoja niweke na mawasiliano hapa
    jokalamdimu@@gmail.com

    tuwasilane mwanvita usiogope kuolewa

    ReplyDelete
  12. mwamvita....mwanya au pengo?

    ReplyDelete
  13. Wajamenituwe na moyo wa huruma kwa kutoa msaada!

    Ibada sio mpaka tuwe ndani ya majengo fulani, Jamii inayo tuzunguka ni moja ya HEKALU KUBWA sana la Ibada na Ibada yenyewe ni kuwajali kwa chochote watoto walio ktk mustakabali wa kimaisha na mazingira kama hawa.

    TUACHE UTAMADUNI NA SILIKA MBAYA NA HARAMU KUTUMIA FEDHA NYINGI KWA ANASA NA ULEVI ILI TUELEKEZE NGUVU HIZO KWENYE JAMII YETU KAMA HIVI HAPA!

    ReplyDelete
  14. mwamvita....mwanya au pengo?

    Mdau huo kwa Mwamvita ni mwanya tena wa juu!

    Kwa wanaojua mipango wanaelewa mtu akiwa na sifa hii anakuwaje?

    Sasa basi inaelekea Wagombea Uraisi Wadau wetu wawili waliojitokeza hadi muda huu kwa Maoni yao kufika bei kwa Binti humu yaani 1.David V na 2.Joka la Mdimu,,,kati ya hao atakaye piga bao atakuwa amepata haswaaa!!!

    ReplyDelete
  15. Mpambano wa kusaka saka kati ya Wadau David V na Joka la Mdimu,,,inabidi Ankal awe ndio Refa wa Mchezo!

    Sisi wengine yetu macho tunasubiri kupewa kadi na kuitwa kwenye mnuso!

    ReplyDelete
  16. Haya Mashemeji watarajiwa Wadau wenzetu David V. na Joka la Mdimu,

    tunasubiri kete zenu kurushwa katika drafti tupate mbivu na mbichi!

    Ila sio siri atakayepata atakuwa amepata!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...