Na Tiganya Vincent-Arusha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete anatarajia kufungua mkutano wa Kimataifa wa Mamlaka za Kuzuia na Kupambana na Rushwa kutoka nchini mbalimbali .
Kauli hiyo imetolewa leo na Msemaji wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU)  Doreen Kapwani wakati wa mahojiano na mwandishi wa habari hizo mjini Arusha.
Kapwani amesema kuwa hii ni mara ya kwanza mkutano wa namna hiyo kufanyika nchini ambapo zaidi ya washiriki 65 kutoka nchi mbalimbali wanatarajia kushiriki mkutano huo wa siku tatu.
Amesema kuwa mkutano huo unatarajia kushirikisha Nchi kama vile Morocco , Uingereza, Qatar, Uganda, Romania, Brazil, Austria, india, Belgium , Spain, Ukraine , Malsiyia , Namibia na Mwenyeji Tanzania.
Kwapwani amesema kuwa mkutano unafanyika hapa nchini wakati Tanzania imepata heshimiwa kubwa ya Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Dk. Edward Hoseah amechaguliwa kuwa Mwenyekiti Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri juu ya Rushwa ya Umoja wa Afrika Machi mwaka huu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...