Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk.Ali Mohamed Shein,akimuapisha Yahya Khamis Hamad,kuwa Katibu wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar, leo baada ya kumteuwa kushika nafasi hiyo. Hafla ya kiapo ilifanyika Ikulu Mjini Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk.Ali Mohamed Shein,akimuapisha Luteni Kanali Mohamed Mwinjuma Kombo,kuwa Mkuu wa Kikosi cha Valantia Zanzibar,jana baada ya kumteuwa kushika nafasi hiyo,hafla ya kiapo ilifanyika Ikulu Mjini Zanzibar.Picha na mdau Ramadhan Othman,Ikulu Zanzibar




neno VALANTIA hapo juu lina maanisha nini wadau ??
ReplyDeleteHilo ni neno lenye sili ya neno la Kiingereza 'volunteer' kwa maana ya 'anayejitolea'. Hata hivyo valanti hapa Zanzibar hufanya kazi zinazofanana na askario wa mgambo huko kwenu ingawa lenyewe siku hizi limepoteza maana halisi tofauti na zamani. Siku hizi valantia ni ajira yenye malipo. i.e. siyo kujitolea tena.
ReplyDeleteHapo ndipo nachanganyikiwa, nani mkuu wa majeshi hapa Tanzania, na ili Valantia ni Jeshi chini ya Mkuu wa Majeshi? maana huyu Luteni Kanali ni Jeshi la Wananchi. Wadau ebu niweke sawa
ReplyDeleteVolunteer walipata sifa sina wakati wa miaka ya 70 kwa ukamataji wa wavaaji wa "Mabugaluu" na "Mini-skirt" na "Afro" na mikanda ya 007.
ReplyDelete