Picha Juu na chini ni Mhe. Mwanaidi Maajar Jumamosi April 28, 2012 alikutana na uongozi mpya wa Jumuiya ya Watanzania DMV katika Ofisi za Ubalozi wetu Jiji Washington viongozi waliochaguliwa kwenye uchaguzi uliokua wa kihistoria ni Rais Iddi Sandaly, Makamu wa Rais Raymond Ibrahim, Katibu Amos Cherehani, Muweka hazina  Genes Malasy na wajumbe wa bodi ni Dr. Hamza Mwamoyo, Al-Amin Chande, Grace Sebo Mgaza, Eliserena Kimolo pamoja na Haruni Ulotu
 Viongozi wa Jumuiya wakipiga picha ya pamoja walipokua Ubalozi wetu jijini Washington, waliokaa kutoka shoto ni Muweka Hazina Genes Malasy, Katibu Amos Cherehani, Rais Iddi Sandaly na Makamu wa Rais Ray Ibrahim na aliosimama kutoka kushoto ni Wajumbe wa Bodi Eliserena Kimolo, Al-Amin Chande, Grace Sebo Mgaza na Dr. Hamza Mwamoyo.
Mhe. Balozi Mwanaidi Maajar katika picha ya pamoja na na uongozi mpya wa Jumuiya ya Wanzania DMV pamoja na maafisa Ubalozi wa Tanzania Nchini Marekani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Mhe. Balozi Mwanaidi S. Maajar , Raisi Mteule wa DMV Mhe. Iddi Sandaly na Uongozi mzima wa Ubalozi na Jumuia kazi kwenu Jumuia ya Watanzania tuna matarajio makubwa kwa mabadiliko na ujio wa Uongozi mpya.

    Kila la kheri!

    ReplyDelete
  2. Hongereni sana viongozi matumaini yangu mtaelekeza nguvu kwenye uwekezaji wa ndani.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...