Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Uwekezaji na Uwezeshaji Dk. Mary Nagu akitoa hotuba yake wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Pili la Makatibu Muhtasi nchini Tanzania (2th National Secretarial Confrerence) linaloendelea hivi sasa kwenye ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Malaika Beach Resort,Jijini Mwanza.
Mkuu wa Mkoa Mwanza,Eng.Evarist Ndikilo akitoa hotuba yake wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Pili la Makatibu Muhtasi nchini Tanzania (2th National Secretarial Confrerence) linaloendelea hivi sasa kwenye ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Malaika Beach Resort,Jijini Mwanza.
Mwenyekiti wa Chama cha Makatibu Muhtasi Tanzania (TAPSEA),Pili Penda akitoa maelezo mafupi ya Kongamano hilo kwa Mgeni rasmi ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Uwekezaji na Uwezeshaji Dk. Mary Nagu wakati wa ufunguzi uliofanyika leo kwenye ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Malaika Beach Resort,Jijini Mwanza.
                   Ephraim Kibonde ambaye ndie Mc wa Kongamano hili akifungua rasmi
Baadhi ya Makatibu Muhtasi waliohudhuria kongamano hili

au 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Kuna pengo kubwa baina ya wanawake na wanaume katika kazi hii ya ukatibu muhtasi!!

    ReplyDelete
  2. hongereni lakini jiendelezeni, maana nyie ndio mnajua ofisi kuliko mabosi wenu na kazi yenu ni makini. Kero yangu ni kwamba hii kazi inaonekana ni ya wanawake anagalia walivyojazana hapo

    ReplyDelete
  3. Nadhani muda si mrefu hata makatibu muhtasi wanaume wataongezeka. Unajua huki cheo kimekuwepo toka kipindi cha mfumo dume wa kiutawala. Wakati huo mabosi wengi walikuwa wanaume. Hao wasichana (makatibu muhtasi)pamoja na kazi nyingine, kazi mojawapo ilikuwa ni ku-take care bosi wa kiume. Kwa ufupi huyu huitwa mke wa pili wa bosi. Baada ya muda kadhaa, anaenda kumuuliza bosi nikuletee nini? Mara anamtengeneza vizuri kola ya shati au tai. Ikibidi hata anampatia kidogo kitumbua chake.

    ReplyDelete
  4. Hawa wana kazi kubwa, kwa kawaida wanatunza kumbukumbu za kampuni. Wanajua kila kinachoendelea na wanajua taratibu za kampuni kuliko baadhi ya mabosi. Waongezwe mshahara na malupulupu, kwa kweli kazi yao ni nzito kuliko watu wengi wa ngazi yao au wengine wenye kazi za kikarani.
    Wengi wamejiendeleza ili kuwa sambamba na technolojia ya electronic. wanaweza kutunza mahesabu na kukusanya takwimu ( database). Wanajua mabo ya human resources na administration kwa ujumla. Mungu awaongezee ushupavu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...