Magari mengi yakiwa yamesimama kwenye foleni kubwa katika njia ya mtaa wa azikiwe street katitaki ya Jiji la Dar wakati huu wa jioni.hali hii imekuja kutokana na mvua kubwa iliyonyesha leo jijini Dar. 
hakuna gari inayosogea hata kwa hatua moja mbele.hapa ni kwenye kip left ya makutano ya Azikiwe na Samora.
 Makutano ya Makunganya na Indra ghand pamoja na Kaluta pia hali ni kama hivi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. duh hatar kubwa thana

    ReplyDelete
  2. Katika maisha ya Dar, kati ya vitu vinavyo sababisha maisha kuwa magumu ni foleni. Foleni ya Dar inarudisha nyuma maendeleo, inawafanya watu wanakosa raha, wanachoka, wanapoteza muda mwingi sana barabarani, wanapoteza hela za ziada kwa sababu ya mafuta ya magari yao, ajali/kupigana pasi, kumkosea muumba wetu maana kuchomekeana kwingi mwishowe kunasababisha hasira na kutoa matusi kwa wingi.

    Hili ni tatizo kubwa ambalo serikali inatakiwa itafute suluhisho la kudumu. Tunapata hasara kubwa sana, ni kwa vile tu hamna utafiti wa kitaalamu ulishafanyika na kuanika ukweli ya hasara zinazopatikana kutokana na foleni hizi. Kuna uwezekano mkubwa wa kutatua hili tatizo ni kiasi cha kutoa kipaumbele hili tatizo. Manuafaa ya kutatua hili tatizo ni mengi sana kulikoni kuendelea kulifumbia macho.

    ReplyDelete
  3. Nafikiri wakati umefika kujengwe "Metro" Dar.

    ReplyDelete
  4. ufumbuzi upo tena wa haraka ofisi za serikali zote zingehamishiwa makao makuu Dodoma na pia iwekwe sheria m'bunge yeyote asiruhusiwe kukaa nje ya jimbo lake, mi naona kwa kiasi flani foleni ya magari itapungua 7bu viongozi hawa na watu wao wa karibu ndio wanaomili magari mengi pia msafara wa raisi itakua hamna mara kwa mara watu wa dar hebu tupambane kwa kufikisha mawazo yetu maana watabomoa nyumba mpaka lini?

    ReplyDelete
  5. HAki Ya nani Tena Bongo Tambarareeee....AhhhAcha Nibebe BOx tu mie...Bongo Nomaaaaaaa!!!

    ReplyDelete
  6. Yani jr jana ilikua balaa,wa kule Kijichi hakuna cha daraja wala barabara.Ilinibidi nikodi chata.

    Mama Mimah!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...