JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA RAIS
SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA
Kumb. Na EA.7/96/01/B/40 30 Machi, 2012
TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI
Sekretariati ya Ajira katika Utumishi wa Umma ni chombo ambacho kimeundwa kwa mujibu wa Sheria ya Utumishi wa Umma Na. 8 ya mwaka 2002 kama ilivyorekebishwa na Sheria Na. 18 ya mwaka 2007 kifungu 29(1).
Kwa mujibu wa Sheria hiyo, chombo hiki, pamoja na kazi zingine kimepewa jukumu la kutangaza nafasi wazi za kazi zinazotokea katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Waajiri (Taasisi za Umma).
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma anakaribisha maombi ya
Watanzania wenye sifa na uwezo wa kujaza nafasi za kazi kwa waajiri mbalimbali katika
Utumishi wa Umma kama ifuatavyo:
JAMANI KAMA HIKI SI KIINI MACHO NI NINI? TANGAZO LINATOLEWA LEO NA KESHO NDO MWISHO WA KUPOKEA MAOMBI NA HAMKUBALI WATU KULETA MAOMBI KWA MKONO NA WALA HAKUNA BARUA PEPE!!! WATU WALIOKO MIKOA TOFAUTI NA DAR ES SALAAM WANAFANYAJE? AU WAO AJIRA HII HAIWAHUSU? UPO UMUHIMU WA KUONGEZA MUDA WA KUPOKEA MAOMBI. TOFAUTI NA HIVYO TUNADANGANYANA TUUU.
ReplyDeleteMUDA MLIOTOA HAUTOSHI, TUACHE KUDANGANYANA. TANGAZO LEO MWISHO WA KUPOKEA MAOMBI KESHO MNAMAANA GANI?
ReplyDeletePOLENI WADAU HAPO JUU, TANGAZO HILI SI KWAMBA LIMETOKA LEO LAA HASHA LILITOKA SIKU NYINGI ILA HAPA KWA MICHUZI NDO LIMEBANDIKWA LEO! POLENI KWA KUKOSA DEADLINE!
ReplyDelete