Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, Mama Salma Kikwete, akiwapa somo la kucheza na kufunga magoli wakati alipowatembelea kwenye kambi yao ya mazoezi wakijiandaa kwa michuano ya Afrika itakayofanyika hapa nchini hivi karibuni.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiangalia mazoezi ya timu ya taifa huko Kibaha walikopiga kambi yao.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akitoa maelekezo kwa wachezaji wa timu ya taifa ya netiboli,Taifa Queens, wakati wakifanya mazoezi kwenye kambi yao iliyoko katika shule ya sekondari ya Philbert Bayi huko Kibaha wakati alipowatembelea
Mwenyekiti wa WAMA, Salma Kikwete, akimkabidhi mchango wa shilingi milioni kumi, Mwenyekiti wa CHANETA, Anna Bayi, kwa ajili ya maandalizi ya timu ya taifa ya mchezo huo. Makabidhiano hayo yalifanyika huko Kibaha tarehe 4.5.2012 ambako timu hiyo imeweka kambi.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa WAMA, Salma Kikwete, akifuatana na wake wa Makamu wa Rais,Zakhia (wa pili) na Asha Bilali (wa mwisho) wakiagana na wachezaji wa timu ya Taifa ya Netiboli huko Kibaha. 
Picha na John Lukuwi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...