Salaam kaka Michuzi,

Naomba unisaidie kutundili hili Bloguni,Maana nina rafiki yangu huwa twawasiliana, anaishi UK. So ametuma parcel kwa kutumia Capacity Cargo Delivery. 

Na akanitumia receipt na tracking number. Nimekuwa nikitruck na kuona kuwa hiyo percel imeshakuwa cleared UK ila itapitia Spain, Malaysia then Tanzania. Inaonyesha kama hivi:

25-05-2012
11:30
                United Kingdom
                  Cleared
26-05-2012
3:20
               Spain
                  Awaiting Arrival
28-05-2012
10:05
               Malaysia
                  Awaiting Arrival
29-05-2012
1:45
                   Tanzania
                  Awaiting Arrival

Sasa kama mnavoona hilo jedwari hapo, halionyeshi so far kama iyo parcel inatembea. Naomba mnisaidie kujua yafuatayo hasa mnaoishi UK

Je hii www.ccdelivery.org ni genuine website?  Na Capacity  Cargo  Delivery ni genuine na reliable company?

Maana nimepigiwa simu toka Malaysia kuwa nitume some amount of money kupokea hiyo parcel ambayo ilishalipiwa malipo ya kutuma toka UK. 

Wasiwasi wangu ni kwanini malipo yaende tena kwa western union wakati kama ni clearance fee basi ikiwa hapa bongo imeshafika naweza tu kwenda na kulipa na kuchukua kama ambavyo nikipokea percel kwa DHL  ninavyofanya.

Na email walonitumia inaonyesha code number ambayo nimewahi kuiona mtu ana complain kuwa Malaysia wameshikilia parcel yake na akawa anauliza whether alipe au asilipe mana nae alikuwa ana wasiwasi. Nami nashindwa kumuuliza alienitumia maana kasafiri.

Naomba msaada kwa waliowahi pitia Capacity Cargo Delivery na kama huo ndo utaratibu maana hata mie ni mara ya kwanza kutumiwa kupitia hiyo. Nahitaji msaada wenu kabla sijafanya maamuzi.

Asante sana
Ni mimi dada yenu
Angela

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 22 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 28, 2012

    DADA ANGELA POLE SANA HIYO NI KANYA BOYA WENZIO WALIFIKA AIRPORT KUSUBIRIA MTU ALIYEMTUMIA PARCEL MPAKA ALIPOGUNDUA NA KUONDOKA BE MAKINI MDAU SOPHIA WA MSASNI.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 28, 2012

    kuwa makini dada mara nyingi hao ni matapeli wasiliana vema na huyo nduguyo kama kweli ametuma hiyo parcel kama ulipata ujumbe kwa mail inawezekana wajanja wamehack email addres yake na kuitumia please kuwa mwangalifu katika mambo kama hayo wengi wamelizwa mpendwa

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 28, 2012

    Habari yako dada, hao ni matapeli ndo huwa wanajifanya hivyo na ukituma hizo walizokuambia utaambiwa utume zingine tena na walivyo washenzi hawataki utume kwenye jina la kampuni hapana wanataka ulipe kwa jina la mtu wanakutajia tena njia ndo hiiyo western union....

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 28, 2012

    huyo alikutumia toka UK anatakiwa aende ofc za hao akawasiliane nao coz walimpa muda wa parcel kufika na sababu atakuwa na risiti. anaweza dai arudishiwe parcel na hela au wakikataa ana haki ya kuwashitaki fairtrade n they will be in shit. thas the only way ila hela usitume hata senti coz its a scam!!

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 28, 2012

    Ni kweli una rafiki yako anaeishi UK? Rafiki wa kwenye mitandao au rafiki unaye mjua au mmeshakutana ana kwa ana. Maana usikute umedanganywa na matapeli ya kinaigeria kwenye mtandao. Mtu akisha kutumia parcel hamna malipo yeyote unayotakiwa kulipia kabla mzigo haujakufikia. Kuwa makini hapo huenda unatapeliwa.

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 28, 2012

    Angalia sana ndungu yangu hapa UK pamejaa Wapopo(Nigerians) Wana makampuni mengi kweli fake ya Kudeliver parcel, wengi wao Wahuni. Wee google kuchek kama ni Scam Companies. Ngoja nianze kukupa Pole

    ReplyDelete
  7. Mdau, GenevaMay 28, 2012

    Dada, kwa hesabu za haraka haraka, hapo ni utapeli mtupu. Ushauri - hakuna cha parcel wala nini na ukituma hela umeliwa!

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 28, 2012

    Pole sana Angela.
    Muhimu hapo ni kuwapigia Capacity Cargo Delivery hapa UK or Main Office na kuwauliza.Endapo umetumiwa mzigo from UK to Tanzania basi freight charge must be from Uk to Tz.Hizo transit hazikuhusu kabsa,wangepitishia Germany,Kenya then Tanzania is up to wao.So just phone them in main Office wape jina la mtumaji na Ref namba ya parcel.Malsiya waizi hapo,wasije kuwa Wapopo(Nigeria )wame truck parcel hiyo.

    ReplyDelete
  9. in my experience anybody asking for money via western union is a scam artist. yaani msaani. dont send money and wait till you can contact your friend and ask him what is really going on.

    ReplyDelete
  10. Mdau, GenevaMay 28, 2012

    Dada, kwa hesabu za haraka haraka, hapo ni utapeli mtupu. Ushauri - hakuna cha parcel wala nini na ukituma hela umeliwa!

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 28, 2012

    Mimi nipo London hizo company ulizotaja sio zakuaminika naona kama kunamchezo hapo kama nikulipia ingetakiwa mzigo ufike Tz ndo wakati unapoendakuupokea ndo ulipe something sio utume hela Malaysia,kua makini dada maisha yamekua magumu kila mahali hivyo watu wanatafuta njia yoyote yakupata hela hata kama sio halali.
    Nawakilisha.
    Mdau london.

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 28, 2012

    Tuwasiliane 0774350355

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 28, 2012

    May 0713225845 na mi yamenikuta hayo nipigie nikufahamishe, ni matapeli kwangu ilikuwa ultimateexpresscourier@asia.com

    ReplyDelete
  14. AnonymousMay 28, 2012

    Asanteni sana jamani mana dah. Ila nsingetuma hadi niwe na uhakika. Ila nawashukuru wadau wa UK kwa ushirikiano na wengine wote.

    ReplyDelete
  15. AnonymousMay 28, 2012

    si umwambie aliyekutumia afatilie huko alipopeleka mzigo na kulipia FULL STOP

    ReplyDelete
  16. AnonymousMay 28, 2012

    Please visit this site for more complaints about capacity cargo delivery. Http://www.consumercomplaints.in/bycompany/capacity-cargo-delivery-a140924.html

    Chonde x99 Dada Yang don't send any penny - utalizwa asubuhix2

    ReplyDelete
  17. AnonymousMay 28, 2012

    NINYI WA TANZANIA MIMI NAONA BADO MNA TONGO TONGO ZA USINGIZI WA 1942,HIVI KWELI WEWE UNAWEZA KUKUTANA NA MTU KWENYE NET ATI MPAKA UKAMPENDA NA AKUTUMIE PARCEL WEWE? YEYE HANA DADA HUKO KWAO HATA KAMA N I MZUNGU AU ANA KASORO AU NI MGONJWA WA UKIMWI ANATAFUTA WATANZANIA WANAWAKE NDIO WAJINGA DUNIANI KWA KUTAPELIWA ,KWA SABABU WANAWAJUENI KANA KWAMBA HAMNA ELIMU . HIO NI NIGERIA CONNECTIO KAMA HAMJUI HIVYO WANAWAKE WENGI WAISHA TAPELIWA NA HAO MA NIGERIA, SHAURI ZENU, NDIO MAANA MNAAMBIWA MBADILISHE SIASA SASA MAANA WENGI WENGI BADO MNAFIKIRI NYERERE BADO YUPO NA TANU AU CCM, ALISHAFARIKI CHAGUA CHADEMA CHAMA CHA KUPANUANA MAWAZO. ACHENI AKILI YA ABOUD JUMBE MJANJA WA UNGUJA MIAKA YA 1960 WAKATI HAKUNA TV ZANZIBAR AKATAPELI HUKO KAWAACHA WATU WAMELALA MPAKA LEO WANA FIKIRI UISLAM NDIO MAISHA, BADALA YA KUSOMA SHULE ZA KISASA WAO MPAKA LEO BADO WANANGANGANA NA MADRASS ETI KUMSOMA NABII WAKATI HATA KUTENGENEZA SINDANO HAWAJUI WALA KULIMA HATA TOMATO KWAO NI NGOMA.

    ReplyDelete
  18. AnonymousMay 28, 2012

    BURE GHALI:

    Kwa nini aliekutumia mzigo asitumie huduma za Kampuni ya kueleweka kama DHL, USPS au FEDEX?

    Tatizo mnabana sana matumizi matokeo yake mnapigwa sasa.

    ReplyDelete
  19. AnonymousMay 29, 2012

    We uliendika na herufi kubwa hapo juu nahisi huna akili nzuri, zimekuruka. Hafu huwezi tofautisha issue moja na nyingine, pia huwezi fikiri kuwa kwa huyu dada kuomba msaada huu inasaidia na wengine kujifunza. Inaonyesha hata utumiaji wako wa keyboard ni wa kudonoa, ndo mana hata unasahau unataka kusema nini. Uwe unakaa kimya kama huezi kuongea sense. Nakushauri urudi darasani kujifunza consistence ya unachokiongea. Sio kila mtu lazima atoe maoni humu, naona wengine wanajifunza tu kuandika.

    ReplyDelete
  20. AnonymousMay 29, 2012

    Wewe uliyeandika in capital letters kama mngelikuwa mmeendelea na kusoma kila krismas mngelikwenda kunywa mbege na kila mkifa lazima mkazikwe migombani ndio mnaona maendeleo hayo. Kumkabili mungu na mini na mpasuo mpaka matakoni huko ni kuendelea na kusoma. Acha ujinga. Kama wewe unaona dini yako ni nzuri na anaeabudu miti na majabali nae pia anaona dini yake ndio ya kweli, vilevile kuna budha nae humwambii. Baniani hapeleki hekalu lake ambapo anajua hakuna waumini.

    ReplyDelete
  21. AnonymousMay 29, 2012

    Santacy Delivery Company ndo ilikuwa yangu hao ni matapeli wa kinigeria kama ulikutana na huyo rafiki yako kwenye mtandao, na sikuwatumia hata senti tano na niliwaambia hizo hela sina na huo mzigo urudishwe kwa muhusika na wanavyojidai kukwambia kuna vitu vya thamani. Nigerian ni wezi wa mitandao hakuna mfano...

    ReplyDelete
  22. Dunia ina wengi!!!

    Dada Angela anaonekana amenaswa na wapopo na bahati yake ameomba msaada tutani.

    Wadau mbalimbali wamajaribu kumfumbua macho dada yetu pamoja nasi wadau wengine kuhusu usanii wa wapopo ulivyomahili.

    Lakini jamani, wadau wengine, TANU, CHADEMA,UISLAMU,ABOUD JUMBE, MADRASS, Krismas, Kuabudu miti, mpasuo matakoni na mbege vina uhusiano gani na hii mada??!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...