Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Severin Tossi(kushoto) akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Njombe John Mahali .Mwenge wa Uhuru umepokelewa leo mkoani Ruvuma katika kijiji cha Ngelenge wilaya ya Ludewa kabla haujaanza mbio zake mkoani Ruvuma.
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kapt.Honest E.Mwanossa akifungua jengo la hosteli ya wasichana katika shule ya sekondari ya Mbambabay wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma.
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2012 Kapt.Honest E.Mwanossa akimsaidia kubeba ndoo ya maji Bi .Hilda Ngoya mkazi wa kijiji cha Nkaya wilaya ya Nyasa mara baada ya kiongozi huyo kuzindua kisima cha maji kilichoghalimu Tsh 14.9 milioni.Mwenge wa Uhuru utakuwepo mkoani Ruvuma kwa siku sita.Picha na Muhidin Amri wa Globu Jamii,Ruvuma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 29, 2012

    Kufungua jengo la hosteli ya wasichana mwaka 2012 kwa kumtwika msichana ndoo ya maji ni kuendelea kumdhalilisha mtoto wa kike na kurudisha nyuma maendeleo ya nchi! Wake up people!!

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 29, 2012

    Hii habari ya mwenge wa uhuru ni miongoni mwa vitu vilivyopitwa na wakati. Ni kuongeza tu matumizi ya serikali yasiyokuwa ya lazima. Badala ya kuzunguka nao kila mwaka pengine ungezuka tu mwaka wa uchaguzi na sensa kuhamasisha watu. Otherwise uwe kimya.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 29, 2012

    hivi mwenge una faida gani,nimekuwa nikisikia bajei kubwa ya mwenge lakini sioni matunda yake,kwani usiwe unakimbizwa kila baada ya miaka kumi hiyo hela yake ikatumika kufanya vitu vingine vya msingi kama vile elimu-kufadhili wanachuo,afya -kujenga majengo na kutoa vifaa vya mahospitalini na kunusuru hawa wanaotuleta duniani wasilale chini kama nyoka.

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 29, 2012

    ulaji wa wajanja huooooooo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...