Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii Mhe. Jenister Mhagama akisisitiza jambo wakati wakipokea makadirio ya bajeti ya wizara ya kazi na Ajira iliyo wasilishwa mbele ya kamati hiyo. Kushoto kwake ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Juma Nkamia na Kulia ni Katibu wa Kamati hiyo Chacha Nyakega, Waziri wa Kazi na Ajira Mhe. Gaudensia Kabaka na naibu waziri wa Wizara ya kazi na Ajira Mhe. Dkt Milton Makongoro Mahanga.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufunzo Mhe. Shukuru Kawambwa akiwasilisha makadirio ya bajeti ya Wizara yake mbele ya Kamati ya Huduma za Jamii kabla ya kupelekwa Bungeni. Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii Mhe. Magareth Sitta na Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Dkt. Faustine Ndugulile.
Makamu Mwenyekiti wa kamati ya Huduma za Jamii Mhe. Faustine Ndugulile (kushoto) na Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Magareth Sitta (katikati) wakimsikiliza kwa makini Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufunzo Mhe. Shukuru Kawambwa alipokuwa akiwasilisha makadirio ya bajeti ya Wizara yake mbele ya kamati hiyo leo.
Mwenyekiti wa Kamati ya fedha na Uchumi Mhe. Andrew Chenge akifafanua jambo mbele ya wajumbe wakamati na watendaji kutoka wizara ya fedha baada ya kupokea mapendekezo ya bajeti ya wizara ya fedha yaliyo wasilishwa mbele ya kamati hiyo leo. Kulia kwake ni Waziri wa fedha Mhe. William Mgimwa Mhe Saada Mkuya Salum na Mhe Janet Mbene, amabo ni Manaibu waziri katika wizara hiyo.
Mjumbe wa kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma Mhe.Murtaza Ally Mangungu akifurahia jambo baada ya kupokea hesabu zilizokaguliwa za chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kwa mwaka 2010/2011. Kulia kwake ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. zitto Kabwe na Kushoto ni Katibu wa Kamati hiyo Erick Maseke
kamati ya POAC ikiendelea na kazi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 07, 2012

    Nawasihi kamati ya POAC msihishie hapo kwenye vyuo vya biashara nendeni hadi kwenye vyuo vya ufundi mkajionee wenyewe.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 07, 2012

    POAC Muende mpaka kwenye vyuo vya ufundi Kama DIT

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 08, 2012

    baada ya kamati kukaa ile bajeti nusu pelekeni makanisanini mkuze nguvu ya imani ya dini yetu

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...