Meneja wa kinywaji cha Konyagi Martha Bangu na Mwnyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Vikunai Zena Khamisi wakifungua bomba la maji kuashiria uzinduzi wa mradi wa kisima cha maji ambacho kimechimbwa na kampuni hiyo Mbagala Vikunai,jijini Dar es Salaam.
Meneja wa kinywaji cha Konyagi Martha Bangu akimtwisha ndoo ya maji mmoja wa wakazi wa Mtaa wa Vikunai kilichopo eneo la Mbagala jijini Dar es Salaam mara baada ya kuzindua kisima cha maji kilichochimbwa na kampuni hiyo.
Maji ni kilio cha muda mrefu kwa wakazi wa eneo hili. Naishukuru kampuni ya Konyagi kwa msaada huu.
ReplyDeleteDkt Faustine Ndugulile
Mbunge Kigamboni
Hiyou sarawili ikilowana je? (kati ya mvua na jua unapenda nini?)
ReplyDeleteHiki isima kingependeza kama kingekuwa kinatoa kinatoa konyagi badala ya maji.
ReplyDeleteNdo maana serikali yetu legelege kwa "wawekezaji". Kwa misaada midogomidogo kama hii basi tunabweteka. hivi kweli serikali inashindwaje kuchimba visima vidogovidogo kama hivi? Unaenda wilayani unakuta Mwenyekiti wa halmashauri na mkurugenzi wanatembelea magari kuanzia sh. 200 milioni kwenda mbele,bei ya kisima kimoja ni sh.20 milioni au chini zaidi lakini wilaya ina shida ya maji kuliko jangwani. Sasa hapo tunasema ni ukosefu wa uwezo kwa serikali kweli? Wananchi inatakiwa sasa tuwawajibishe viongozi wetu,wanatutesa sana.
ReplyDelete