AL HABIB MICHUZI
Sabal Khayr.
Mimi naomba nishauri kuwa kama mtu anatuma shairi basi iwe kwa maximum beti ziwe 3 ili iwe rahisi kwa msomaji .Pia sharti lingine Shairi shurti liwe ni kiswahili sanifu ili kuondoa wanaoharibu lugha (lisiwe na kiingereza). Muhimu pia mtu aelezee kwa nini anaandika hilo shairi.Mimi bado nasubiri majibu toka kwa huyo niliyemwomba Mkopo kwenye shairi la MKOPAJI
Na kama ni swali limeulizwa basi si haba shairi likawa juu ya habari kwa masaa 24 kama hakuna majibu basi habari zingine zifuate lakini majibu yakitolewa basi si haba kama yakawa juu
Natumai Malenga wenzangu wataunga mkono hoja
-Wimbi la mbele
Hili nalo ni shairi la Muyaka bin Hahi al Ghassay wa Voi Kenya na aliliandika kwenye karne ya 18. Kwa sasa nitatoa beti 2 tu lakini mshairi anazungumzia kutendeana wema:
Akutendeae Mema
Kumsuhuru ni lazima
Jaza ya mema ni mema
Maovu Umeyatia
Mbona umeghafilika?
Kwa jambo lisilo na shaka?
Shetani umemshika
Umemwacha nabia.
Sabal Khayr.
Mimi naomba nishauri kuwa kama mtu anatuma shairi basi iwe kwa maximum beti ziwe 3 ili iwe rahisi kwa msomaji .Pia sharti lingine Shairi shurti liwe ni kiswahili sanifu ili kuondoa wanaoharibu lugha (lisiwe na kiingereza). Muhimu pia mtu aelezee kwa nini anaandika hilo shairi.Mimi bado nasubiri majibu toka kwa huyo niliyemwomba Mkopo kwenye shairi la MKOPAJI
Na kama ni swali limeulizwa basi si haba shairi likawa juu ya habari kwa masaa 24 kama hakuna majibu basi habari zingine zifuate lakini majibu yakitolewa basi si haba kama yakawa juu
Natumai Malenga wenzangu wataunga mkono hoja
-Wimbi la mbele
Hili nalo ni shairi la Muyaka bin Hahi al Ghassay wa Voi Kenya na aliliandika kwenye karne ya 18. Kwa sasa nitatoa beti 2 tu lakini mshairi anazungumzia kutendeana wema:
Akutendeae Mema
Kumsuhuru ni lazima
Jaza ya mema ni mema
Maovu Umeyatia
Mbona umeghafilika?
Kwa jambo lisilo na shaka?
Shetani umemshika
Umemwacha nabia.
mashallah shairi zuri na limepoa na ni kweli wengi wetu tumeshika shetani tumemuacha rababa na nabiya
ReplyDeletebwana michuzi, habari navutiwa na uwanja wako ni mpana na wenye njia nyingi za kupitia ahsante kwa kuwapa watu sehemu ya kukutana na kuzungumzia yao na yetu pia. mimi nimpenzi wa blog hii nataka kutoa ushauri kwa mshairi aliyeomba mkopo,amejieleza vyema ila tena aliporudi akishauri watungaki watunge alau beti mbili au tatu na pia waelezee maudhuina dhamira hakisi za tungo zao, hapo aaaah, sikumuelewa ushairi wa sasa ndiyo unaojifunua hadi kujua mradi wa mtunzi.Si dhamira yangu kumuumiza mtoa maoni la hasha,tunafurahishwa na mashairi ya watunzi wa njia za kizamani,ukune kichwa hadi upate maudhui ya mtunzi.Shairi la juzi hapa linalohusu sensa mbona lilikuwa zurisana je lingekuwa beti tatu lingejitosheleza kweli? hamu isingekwisha,lakini maoni yangu angalau basi beti nane hadi kumi zitatosha.Huu si ugonvi ni maoni yangu tu sikusudii kumkwaza yoyote.Nawatakieni kila la kheri.
ReplyDeletemdau
Bashir kigamboni
Kila mema anotenda, thawabuze azichuma,
ReplyDeleteDini zote hebu randa, wema himizwa lazima,
Tenda wema kisha nenda, shukurani si lazima,
Kinyume anaekwenda, anamuudhi KARIMA,
Mkopaji:
ReplyDeleteNi muhimu ukajibiwa kwa misitari mirefu ili upashwe ukorofi wako wakati ukidaiwa kulipa deni la Mkopo.
1.Kumbuka ya kuwa Kukopa kutamu kama asali kulipa kuhcungu kama Shubiri !!!
2.Kumbuka kuwa wewe Mkopaji unakmfuata Mkopeshaji ukiwa Mstaarabu lakini wakati ukitakiwa malipo unakuwa mbogo na mkorofi !
3.Kumbuka kuwa ewe Mkopaji unamfuata Mkopeshaji ukiwa Bwege mtozeni, ukifanikisha kupewa mkopo wakati wa kudaiwa unakuwa unaijua sana Sheria ya Mikataba !!!
Ahhh, Ubinaadamu Kazi !