Mahakama Kuu kanda ya Dar es Salaam Octoba 30, 2012 mwaka huu itasoma hukumu ya washitakiwa wanaodaiwa kumuua Marehemu Swetu Fundikira. Washitakiwa hao ambao ni Rhoda Robart askari wa JKT, Ally Ngumbe wa JWTZ na Mohamed Rashid mtumishi wa JKT.

Upande wa mashitaka katika kesi hiyo uliwasilisha vielelezo viwili na mashahidi sita akiwemo daktari aliyechunguza mwili wa marehemu na Benedict Kinyaiya ambaye ni mtangazaji wa TBC.

Washitakiwa kwa upande wao hawakuwa na shahidi walitoa ushahidi wao wenyewe baada ya kukutwa na kesi ya kujibu katika kesi hiyo ya kuua kwa kukusudia.

Wazee wa baraza katika maamuzi yao yaliyotolewa leo, walisema kuwa wanaona washitakiwa hao watatu hawana hatia na hivyo waachiwe.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 14, 2012

    Majuto ni Mjukuu, naamini mnatamani kama ingewezekana kurudisha/reverse tukio mngefanya hivyo but it is too late. Najua mnasikitika kufupisha maisha ya mtanzania mwenzeni kwa titu ambacho mngeweza kutengeneza au kununua tena.

    Dunia tunapita tupendane wabongo japo kiduchu.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 14, 2012

    Hee wazee wa baraza wanaona waheshimiwa hawana hatia...

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 14, 2012

    Ndio maana kabla ya tendo lolote au kauli fikiria kwanza!

    Usipofuata kanuni hii mara zote ndio utakuta watu wamesha kwama na hawan uwezo wa kujikwamua kama hawa wauaji!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 14, 2012

    Umwamba, mabavu na ubabe una hasara zake ndio kama hawa Maafande mambo yaliyowafika!

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 14, 2012

    Waachwie? Ili baraza linamaana gani?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...