Mwanamuziki mahiri kutoka nchini Uganda, Joseph Mayanja 'Jose Chameleone' usiku wa kuamkia leo amefunika vilivyo katika Tamasha la Usiku wa Matumaini lililofanyika ndani ya Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Chameleone aliwarusha mashabiki kwa baadhi ya nyimbo zake za zamani kama Mambo bado, Kipepeo na ile mpya iitwayo Valu Valu inayopendwa na watu wengi hapa Bongo.
Chameleone akiingia uwanjani kuwarusha mashabiki waliofurika Uwanja wa Taifa usiku huu.
Jose akiimba na maelfu ya wapenzi wa burudani waliofurika ndani ya Uwanja wa Taifa usiku huu.
Sehemu ya maelfu ya wakazi wa jiji la Dar waliokuwa wanafuatilia shoo hiyo. Picha zote na  GPL

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 08, 2012

    Hivi ni kwa nini katika mikusanyiko kama hii akina dada huwa wachache mno? angalia picha zote hizo halafu ona ni akina dada wangapi wapo humo.

    Jee ni nini sababu hasa? wanaogopa kwa sababu za usalama wao? hawapendi aina hii ya muziki? hawawezi bei za kiingilio? wazazi na wapenzi wao hawawaruhusu? au ni nini hasa?

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 08, 2012

    Jose Chameleone wewe ni king wa muziki Haki ya mama!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 08, 2012

    Siku zote kimaumbile wanawake na wanaume ni tofauti,kwa hiyo na hisia zao ni tofauti,,vitu kama hivi vijana wengi wa kiume ndo washabiki,na ukilinganisha kuwa watumbwizaji ni wavulana,,hapo kama angekuja Beyonce au Nyota Njema sijui nyota njema yule dada wa Kenya,,wewe ungeona wasichana kibao hapo
    Na pia jambo jingine,,sana sana show za uwazi hivyo kama uwanjani kina dada huwa hawapendi,,wewe angalia kama katika maharusi au clubs ndo kuna msanii yeyote awe hata mvulana utawaona kina dada maana huwa wanapenda sana sehemu za heshima,,hapo wapo,ila sio wengi,,waliokuwepo wamekubuu
    Ahlam,,London

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 09, 2012

    Kina dada wanaogopa kubakwa. Si unajua jamii yetu bado ustaraabu mdogo kidogo.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 09, 2012

    VALU VALU(Walu walu?)

    David V

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 09, 2012

    naomba nikujibu anonymous wa Sun Jul 08, 01:48:00 PM 2012 ni kwamba sio kwamba wadada wengi hatupendi ila bado kuna mfumo dume kwenye jamii zetu...ya kwamba hata ruhusa ya kwenda huko hatupati..wazazi wetu,wapenzi wetu wamekuwa na ugumu wa kutupa ruhusa za kwenda maeneo kama hayo kwa sababu tofauti tofauti..na sababu nyingine ni kuhofia usalama! bado hakuna usalama mzuri pale uwanjani..

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 09, 2012

    wakina dada hawapendi kudhalilishwa na hata hivyo mzazi gani amruhusu binti yake usiku kama wanabakwa mchan kweupe je usiku itakuwaje

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...