LEKA DUTIGITE KIGOMA.. ni tamasha kubwa linalotarajiwa kufanyika mkoani Kigoma  tarehe 17 ndani ya mwezi huu wa saba na kuwashwa moto na wasanii  wazawa wa kigoma. Mpaka sasa ari waliyonayo wasanii  hao ni ya kubwa mno.. mpaka imekuwa kama ni changamoto kwa wasanii wanaotoka katika mikoa mingine, na kulowea zaidi Dar es Salaam. Hata hivyo breaking news inaonyesha kuwa karibia nusu ya nyimbo zinazofanya vizuri hivi  sasa katika soko la muziki hapa nchini ni za wasanii wanaotoka katika mkoa wa kigoma. Angalia nyimbo kama "Kichwa kinauma" yake Ali Kiba aliyomshirikisha Jaydee, "Upepo" Recho, "Mawazo" Diamond, "Maneno maneno" Queen Darleen, "Jua ni wewe" Mwasiti akimshirikisha Ally Nipishe, Na nyingine nyingi kutoka kwa wasanii wao kina Chege, Abdu Kiba, Baba Levo, Makomandoo Bongo, Linex, Banana Zorro na wengine wengi.
























Jambo lingine la kutia hamasa ni jinsi Mbunge wao wa Kigoma Zitto Kabwe anavyoshirikiana nao katika kila jambo. Naye msimamizi wa ama mratibu wa tamasha hilo Mwasiti Almas naye alifunguka na kusema haya "Kila kitu kwetu kama wasanii wa Kigoma kiko tayari kwa ajili ya tamasha hili, Kilichobaki ni wasanii wenyewe kufika mkoani kwao na kutimiza lengo la Tamasha hili, kwani tamasha hili linasimama kuwatia chachu ama hamasa vijana wa mkoa wa Kigoma mkoani humo".

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 14, 2012

    keeep it up zitto...

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 14, 2012

    ZITTO ANAKUNYWA POMBE MUISLAMU WA NGUVU HAYA WATU WA KIGOMA

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 14, 2012

    Zitto naye anavaa saa ya dhababu, nini?

    ReplyDelete
  4. Hata kama niko USA kwa sasa wala sijakulia Kigoma ila mimi ni "muha" kwa kabila, manyovu Kasulu ndiko waliko babu zangu. Nimefurahishwa sana na hii kitu, tuendelee kusupport tulikotoka ukizingatia Kgm ni mkoa uliosahaulika kidogo na wasanii wa sehemu zingine wachukue hii as a challenge. Here we go Kigomans. ONE ORIGIN, ONE LOVE, ONE NATION.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 15, 2012

    Chezeya Ruge, wasanii , hamna pa kukimbilia, Mkipigia debe CHadema Ruge yupo,Mkipigia CCM RUge yupo, kazi kwenu!

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 15, 2012

    HAYA BAHARIA KHAMSIN UMEWACHOKOZA WENZIO SASA UTAWABEBEA MBELEKO GANI MBINU ZA MIKOA

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 15, 2012

    Mdau wa Sat Jul 14, 08:47:00 PM 2012, acha ushamba. Hiyo sio pombe. Ni juice ya Apple, acha kujaji a book from its cover.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 15, 2012

    msimsahau mzee Bichuka wa Sikinde, Zahoro bangwe na wengine wengi pia wanatoka kigoma
    ila wengine wenu hapo mnatoka kigoma ya upande wa pili nna maana ya rwanda na burundi

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 15, 2012

    Juice ya apple haina povu,I would not care less about what the guys drinks, hata kama anakunywa "kinibu", hayo ni maamuzi yake.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 16, 2012

    Mdau kunywa Malta apple uone povu lake hata la safari cha mtoto kama kitu hujui funga mdomo. unaokena wewe ni mrugaruga.

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 17, 2012

    huyo bwanawa kwanza issue iyoko hapa ni ya watoto wa kigoma, yeye analeta bombe na uislaam, uislam umekaza pombe kwa kuwa waislam wapo wanaokunjwa. nakuambia mtakoma kwa mfumo.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...