Ankal Habari..!
Katika harakati za kuimarisha zoezi la ukataji tiketi za treni ya abiria Menejimenti ya Kampuni ya Reli Tanzania _TRL imetoa
Mwongozo ufuatao:
TUNAPENDA KUWAFAHAMISHA WATEJA WETU KWAMBA, KUANZIA JUMATATU JULAI 16, 2012 MTEJA YEYOTE ANAYETAKA KUNUNUA TIKETI YA TRENI LAZIMA AONESHE KITAMBULISHO CHAKE KWA KARANI MUUZA TIKETI BILA HIVYO HATUTAWEZA KUMHUDUMIA.
VITAMBULISHO VINAVYOTAMBULIKA NI VIFUATAVYO; KITAMBULISHO CHA KUPIGIA KURA, LESENI MPYA YA UDEREVA, KITAMBULISHO CHA MUAJIRI, HATI YA KUSAFIRIA, KITAMBULISHO CHA SHULE, BARUA KUITOKA KWA MWENYEKITI WA SERIKALI YA MITAA NAKADHALIKA UTARATIBU HUU MPYA NI KWA AJILI YA KUONGEZA UFANISI NA KUBORESHA HUDUMA ZETU KWA WATEJA WETU!
IMETOLEWA NA MENEJA UHUSIANO ( MIDLADJY MAEZ) KWA NIABA YA KAIMU MKURUGENZI MTENDAJI WA TRL MHANDISI KIPALLO AMAN KISAMFU
DAR ES SALAAM


Hapa ni ukiritimba tu unaongezwa hakuna kuboresha chochote wakati inatambulika kwamba ni wananchi wachache sana wenye vitambulisho maana usafiri huu unatumiwa na watu masikini mno wa vijijini kwa kuwa ni wa bei rahisi, sidhani kama itasaidia au itaongeza adha tu.
ReplyDeleteKweli hili shirika limeishiwa sera,sasa kitambulisho cha nini mimi nataka kusafiri ndani ya nchi?kwahiyo kama sina kitambulisho sisafiri na hizo treni zenu?halafu inasaidia nini au inapunguza nini?sioni maana yake kabisa, ma vitambulisho ya kutengenezesha hapo mjini kibao, mnamashine yoyote ya ku scan hivyo vitambulisho kujua kipi ni halali kipi ni feki?kupotezeana muda tu na kujifanya muonekane mnafanya kazi, mwakyembe hebu dili nao hao, sisi zamani tulikua tunapanda treni bila masharti natulikua tunaenjoy safari ya kigoma. jipangeni upya,mmechemsha kwa hilo.
ReplyDelete