ROBO FAINALI COPA COCA-COLA 2012

Robo Fainali ya michuano ya Copa Coca-Cola 2012 inayokutanisha vijana wenye umri chini ya miaka 17 inaanza kesho (Julai 10 mwaka huu) kwa timu nne kuumana kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salam.

Temeke na Mjini Magharibi ndizo zitakazocheza robo fainali ya kwanza kuanzia saa 2.30 asubuhi. Mara iliyoivua ubingwa Kigoma itacheza robo fainali ya pili dhidi ya Morogoro kwenye uwanja huo huo.

Robo Fainali ya tatu itachezwa keshokutwa (Julai 11 mwaka huu) kwa kuzikutanisha timu za Kinondoni na Mwanza. Mechi hiyo itaanza saa 2.30 asubuhi na kufuatiwa na nyingine kati ya Dodoma na Tanga itakayoanza 10 kamili jioni.

Nusu fainali ya michuano hiyo iliyoanza Juni 24 mwaka huu katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani ikishirikisha timu 28 itafanyika Julai 13 mwaka huu kwenye uwanja huo huo.

Mshindi wa mechi kati ya Temeke na Mjini Magharibi, na Kinondoni dhidi ya Mwanza ndiyo watakaocheza nusu fainali ya kwanza. Nusu fainali ya pili itakuwa mshindi wa mechi ya Mara na Morogoro dhidi ya mshindi wa mechi ya Dodoma na Tanga.

Fainali itafanyika Jumapili (Julai 15 mwaka huu). Mechi zote kuanzia hatua ya robo fainali hadi fainali zitafanyika kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...